Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Michezo Biashara United kupanda ndege kimataifa mwakani
Michezo

Biashara United kupanda ndege kimataifa mwakani

Spread the love

 

KLABU ya Biashara United, kutoka Mara imefanikiwa kushiriki michuano ya kimataifa kwa msimu ujao, mara baada ya kumaliza katika nafasi ya nne kwenye msimamo wa Ligi. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Kwa sasa Biashara United ina pointi 50, kufuatia kupata matokeo ya sare ya bao 1-1, kwenye mchezo wa jana dhidi ya Tanzania Prisons, pointi ambazo hazotaweka kufikiwa na KMC ambao wapo kwenye nafasi ya tano wakiwa na alama 45, huku ukisalia mchezo mmoja.

Biashara United inashikili michuano hiyo, kufuatia Tanzania kupata ushiriki wa timu nne kwenye msimu ujao wa mashindano ya kimataifa.

Klabu hiyo inakamilisha idadi ya timu nne zitakazokwenda kushiriki michuano ya kimataifa mwakani, sambamba na klabu za Yanga, Simba na Azam FC ambazo zimemalizika kwenye nafasi tatu za juu.

Katika timu hizo nne Simba na Yanga zitakwenda kucheza Ligi ya Mabingwa Afrika, huku Azam FC na Biashara zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho.

Hii itakuwa mara ya kwanza kwa Biashara United kushiriki michuano ya kimataifa toka ilipopanda daraja misimu miwili iliyopita.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!