Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Rais Mstaafu Jakaya Kikwete (kushoto ) akisalimiana na Madaraka Nyerere ambae ni mtoto wa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alipowasili Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa ajili ya uzinduzi wa Kongamano la 13 la Kigoda cha Mwalimu Nyerere uliofanyika leo chuoni hapo.
BENKI ya Taifa ya Biashara (NBC) imeshiriki kwenye uzinduzi wa Kongamano la 13 la Kigoda Cha Mwalimu Nyerere uliofanyika leo tarehe 8 Juni, 2022 katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM). Kongamano hilo la siku tatu limezinduliwa na Mkuu wa Chuo hicho, Rais Mstaafu wa Awamu ya Jakaya Kikwete, ambaye aliongoza viongozi mbalimbali wa kisiasa, kitaaluma na kiserikali akiwemo Waziri Mkuu mstaafu Mizengo Pinda. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Mbali na kuwa mmoja wa wadhamini muhimu katika kongamano hilo, Benki ya NBC kupitia tawi lake la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam iliandaa banda maalum kwa ajili ya kutoa huduma zake kwa washiriki wa kongamano hilo sambamba na kushiriki katika kongamano hilo.
“Benki ya NBC tunatambua mchango na falsafa za Hayati Mwalimu Julius Nyerere si tu kitaifa bali pia katika uanzishwaji wa benki hii. Hii imekuwa ni moja ya sababu muhimu kabisa ya sisi kuendelea kuwa mstari wa mbele katika kufanikisha na kushiriki katika masuala yote yanayohusiana na Hayati Mwalimu Julius Nyerere likiwemo Kongamano hili muhimu,’’ alisema Anne Mwaisaka, Meneja wa Benki ya NBC Tawi la chuo hicho.
Leave a comment