Akizungumza katika hafla hiyo, mratibu wa miradi ya WB ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na
Wakala wa Barabara Vijijini – The Rural and Urban Roads Agency (Tarura), Mhandisi Humphrey Kanyenye, ameeleza kuwa fedha hizo zitatumika katika awamu ya pili ya mradi.
Alisema, “katika jitihada za kuboresha miundombinu mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam, Serikali imetia saini mradi wa uendelezaji wa jiji hilo kwa awamu ya pili ambapo utagharimu takribani Sh. 800 biliioni.
“Fedha hizo zimewekewa kipaumbele kwenye miundombinu ya barabara, masoko na uondoshaji wa taka ngumu zinazozalishwa kwenye masoko.”
Akishuhudia utiaji saini huo, Waziri wa nchi ofisi ya Rais tawala za mikoa na serikali za mitaa Angellah Kairuki, amewataka wakandarasi hao waliotia saini kutekeleza mradi kwa wakati.
Waziri Kairuki alisema, “tunategemea mtajifunza katika awamu ya kwanza, na sitegemei kuona makosa ya kwanza yanajirudia. Mjue mmekopa na tunatarajia kuwa mradi huu utaenda kwa wakati na utamalizika kwa wakati. Mtakapoenda kinyume, tutarudi kwenye mkataba unavyosema.”
Kwa mujibu wa serikali ya Tanzania, utekelezaji wa miradi hiyo, utarajiwa kuanza Aprili mwaka kesho, ambapo asilimia 74 ya fedha zitatumika kukarabati barabara, mifereji, maeneo ya wazi, masoko, vituo vya mabasi, kurekebisha miundombinu ya taka ngumu na kujengea uwezo kwa halmashauri za jijini la Dar es Salaam.
Rekodi zilizopo jijini Dar es Salaam zinaonyesha kuwa awamu ya kwanza ya mradi huo, ulitekelezwa katika halmashauri zote tano za jiji la Dar es Salaam, ambazo ni Kinondoni, Ubungo, Temeke, Ilala na Kigamboni.
Leave a comment