Tuesday , 26 September 2023
Home Habari Mchanganyiko Benki ya dunia yamwaga Sh. 800 bilioni kuboresha miundombinu Dar es Salaam
Habari Mchanganyiko

Benki ya dunia yamwaga Sh. 800 bilioni kuboresha miundombinu Dar es Salaam

Muonekano wa jiji la Dar es Salaam
Spread the love
SERIKALI ya Tanzania na Benki ya Dunia (WB), wamejifunga kwenye mkataba wa utekelezaji awamu ya pili ya uboreshaji wa miundo mbinu jijini Dar es Salaam (DMDP 2), utakaogharimu takribani Sh. 800 bilioni. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Akizungumza katika hafla hiyo, mratibu wa miradi ya WB ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na

Wakala wa Barabara Vijijini – The Rural and Urban Roads Agency (Tarura), Mhandisi Humphrey Kanyenye, ameeleza kuwa fedha hizo zitatumika katika awamu ya pili ya mradi.

Alisema, “katika jitihada za kuboresha miundombinu mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam, Serikali imetia saini mradi wa uendelezaji wa jiji hilo kwa awamu ya pili ambapo utagharimu takribani Sh. 800 biliioni.

“Fedha hizo zimewekewa kipaumbele kwenye miundombinu ya barabara, masoko na uondoshaji wa taka ngumu zinazozalishwa kwenye masoko.”

Akishuhudia utiaji saini huo, Waziri wa nchi ofisi ya Rais tawala za mikoa na serikali za mitaa Angellah Kairuki, amewataka wakandarasi hao waliotia saini kutekeleza mradi kwa wakati.

Waziri Kairuki alisema, “tunategemea mtajifunza katika awamu ya kwanza, na sitegemei kuona makosa ya kwanza yanajirudia. Mjue mmekopa na tunatarajia kuwa mradi huu utaenda kwa wakati na utamalizika kwa wakati. Mtakapoenda kinyume, tutarudi kwenye mkataba unavyosema.”

Kwa mujibu wa serikali ya Tanzania, utekelezaji wa miradi hiyo, utarajiwa kuanza  Aprili mwaka kesho, ambapo asilimia 74 ya fedha zitatumika kukarabati barabara, mifereji, maeneo ya wazi, masoko, vituo vya mabasi, kurekebisha miundombinu ya taka ngumu na kujengea uwezo kwa halmashauri za jijini la Dar es Salaam.

Rekodi zilizopo jijini Dar es Salaam zinaonyesha kuwa awamu ya kwanza ya mradi huo, ulitekelezwa katika halmashauri zote tano za jiji la Dar es Salaam, ambazo ni Kinondoni, Ubungo, Temeke, Ilala na Kigamboni.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Rais Samia apewa tano ujenzi barabara Mtwara

Spread the loveWANANCHI wa Mkoa wa Mtwara, wameishukuru Serikali ya Rais Dk....

BiasharaHabari Mchanganyiko

Serikali kununua mitambo 15 ya kuchoronga miamba

Spread the loveSerikali kupitia Wizara ya Madini imepanga kununua mitambo 15 ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Mtanzania aweka rekodi kimataifa kwa kiwanda cha kusafisha dhahabu

Spread the loveIMEELEZWA kuwa Kiwanda cha Kusafisha dhahabu cha Geita Gold Refinery...

Habari Mchanganyiko

MAIPAC kusaidia Kompyuta shule ya Arusha Alliance

Spread the loveTaasisi ya Wanahabari ya kusaidia Jamii za pembezoni (MAIPAC) imeahidi...

error: Content is protected !!