Tuesday , 3 October 2023
Home Habari Mchanganyiko Benki 5 zalimwa faini Bil 1.8
Habari Mchanganyiko

Benki 5 zalimwa faini Bil 1.8

Benki Kuu ya Tanzania (BoT)
Spread the love

BENKI Kuu ya Tanzania (BoT), imezipiga faini benki tano kwa ukiukwaji wa kanuni za Sheria ya Utakatishaji Fedha Haramu. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na BoT tarehe 19 Septemba 2019, inaeleza kwamba benki hizo zimekiuka kauni tatu za sheria ya utakatishaji fedha haramu, ambazo ni namba 17, 22 na 28. Kwa kushindwa kuwasilisha ripoti ya wateja zake, katika Kitengo cha Kudhibiti Fedha Haramu (FIU).

Benki zilizopigwa faini ni African Banking Corparation (T) Limited iliyotozwa faini ya Sh. 145 milioni, Equity Bank Tanzania Limited (580 milioni), I&M (T) Limited (655 milioni), UBL Bank (T) Limited (325 milioni) na Habib African Bank Limited (175 milioni.)

Taarifa hiyo ya BoT inaeleza kwamba benki hizo zinatakiwa kulipa faini husika katika kipindi cha miezi mitatu tangu tarehe waliyopigwa faini.

BoT imezitaka benki na taasisi za fedha nchini kufuata sheria na kanuni zilizowekwa katika utekelezaji w amajukumu yao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wawili wanaswa wakitengeneza noti bandia

Spread the loveJESHI la Polisi mkoani Songwe limewakamata watu wawili kwa tuhuza...

AfyaHabari Mchanganyiko

Chanjo mpya ya malaria Sh 5,000-10,000

Spread the loveShirika la afya la Duniani (WHO) limeridhia chanjo ya pili...

AfyaHabari Mchanganyiko

Wagonjwa kiharusi waongezeka, Hospitali Mkapa yaja matibabu mapya

Spread the loveHOSPITALI ya Benjamini Mkapa kwa kushirikiana na madaktari Bingwa kutoka...

Habari Mchanganyiko

Wananchi waamua kujenga zahanati kukwepa adha kufuata huduma mbali

Spread the loveWANANCHI wa Kijiji cha Kwikerege, kilichopo katika Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!