Saturday , 25 March 2023
Home Kitengo Michezo Beki wa zamani wa Liverpool atua Ikulu Zanzibar
MichezoTangulizi

Beki wa zamani wa Liverpool atua Ikulu Zanzibar

Rais Dk Hussein Mwinyi (kulia) akimkabidhi zawadi Mamadou Sakho (katikati) mara baada ya kumtembelea Ikulu visiwani Zanzibar
Spread the love

Beki wa zamani wa Liverpool na klabu ya Crystal Palace kwa sasa Mamadou Sakho amekutana na Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Dk. Hussen Mwinyi leo Ikuru visiwani humo na kufanya mazungumzo kuhusu kukuza michezo visiwani humo. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea)

Sakho amekuja katika mapumziko nchini mara baada ya msimu wa Ligi Kuu England kumalizika akiambatana na familia yake.

Katika mazungumzo yake na mchezaji huyo Rais Mwinyialisema kuwa wamekubaliana kwa pamoja na Sakho kuanzisha kituo cha michezo cha watoto kitakacho wapa fursa vijana wengi visiwano humo.

“Nimefurahi uwepo wako na tupo tayari kushirikiana nawe kuanzisha kituo cha michezo cha watoto, tuwape vijana wetu nafasi.”alisema Dk Mwinyi

Katika hatua nyingine mchezaji huyo amekubali ombi la bodi ya utalii Tanzania (TTB) kuwa balozi wa Hiyari wa utalii wa Tanzania wakati alipokutana na Betrita Lyimo ambaye ni kaimu mkurugezni mkuu wa bodi hiyo katika hifadhi ya bonde la Ngorongoro.

Kufuatia kukubali ombi hilo tayari timu ya waandishi wa habari wa Televishen ya TF1 ya nchini Ufaransa imewalisili pia nchini Tanzania tarehe 27/5/2021 kwa lengo la kutengeneza makala maalumu ya ziara ya Mamadou itakayotumika kutangaza Utalii wa Tanzania kwenye Soko la Utalii la Ufaransa hususani maeneo yote ya vivutio vya utalii aliyotembelea.

Mchezaji huyo alifika nchini toka tarehe 26 Mei, 2021 kwa ajili ya mapumziko ya siku 10, akiwa na familia yake na kutembelea vivutio mbalimbali vya utalii ikiwemo hifadhi ya Taifa ya Serengeti, Kijiji cha wamasai na seneto pamoja na visiwa vya Zanzibar.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Yanga: Fedha za Rais Samia zinaleta ari kubwa

Spread the loveUONGOZI wa klabu ya Yanga, umesema fedha zinazotolewa na Rais...

Michezo

Simba Sc. yamvulia kofia Rais Samia, yamuahidi makubwa dhidi ya Horoya

Spread the loveWAKATI timu ya Simba ikiibuka na ushindi wa bao 3-0...

Habari MchanganyikoTangulizi

Rais Samia ampandisha cheo RPC wa Dar

Spread the loveMKUU wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Camillus Wambura, amesema...

Habari za SiasaTangulizi

Wanachama 384 CUF watimkia Chadema, Mbowe awapokea, Kambaya ndani…

Spread the loveJUMLA ya wanachama 384 wanachama wa Chama cha Wananchi CUF...

error: Content is protected !!