Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Bei za vifaa vya ujenzi kikwazo makazi bora
Habari Mchanganyiko

Bei za vifaa vya ujenzi kikwazo makazi bora

Baadhi ya vifaa vya ujenzi
Spread the love

MBUNGE wa Viti Maalum, Upendo Peneza (Chadema) ameitaka serikali iangalie uwezekano wa kupunguza kodi katika vifaa vya ujenzi ili wananchi waweze kujenga nyumba bora, anaandika Dany Tibason.

Pia mbunge huyo katika maswali ya nyongeza alihoji ni lini serikali itarekebisha sheria ya madini ili wale wanaopisha sehemu zenye madini ili kuhakikisha wanapatiwa madai yao stahiki bila kupunjwa.

Awali katika swali la msingi la mbunge huyo, alitaka kujua serikali ina mkakati gani kuhakikisha wananchi wanapata makazi bora.

“Tatizo la makazi duni kwa wananchi husababisha afya mbovu na hivyo kupunguza nguvu ya uzalishaji je serikali ina mkakati gani kuhakikisha wananchi wanapata makazi bora,” alihoji Peneza.

Akijibu maswali hayo Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angella Mabura amesema suala la kupunguza kodi ya vifaa vya ujenzi linatakiwa kupitiwa upya ili kuondokana na mkanganyiko ambao unaweza kujitokeza.

Amesema suala hilo la kupunguza kodi ya vifaa vya ujenzi lilijadiliwa lakini ilionekana kuwepo katika mkanganyiko kutokana na kuwepo kwa punguzo katika shirika la nyumba.

Kuhusu sheria ya madini, Mabura amesema sheria hiyo ipo vizuri lakini imekuwa ikitekelezwa vibaya kwa wanaoisimamia na serikali itahakikisha inasimamia haki na sheria hiyo.

Mbali na hilo Mabura amesema serikali inatoa rai kwa mamlaka za serikali za mitaa kutenga fedha za kutosha katika bajeti zao kila mwaka kwa ajili ya kuongeza kiasi cha kupima, kupanga na kumilikisha ardhi katika maeneo yao ili kuwawezesha wananchi kupata makazi bora.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

Habari Mchanganyiko

NMB yafuturisha Dar, Majaliwa azitaka Serikali za Mitaa, Taasisi zijifunze kwao

Spread the loveBENKI ya NMB imewafuturisha wateja wake walio kwenye Mfungo wa...

error: Content is protected !!