MKUU wa Wilaya ya Korogwe mkoani Tanga, Basilla Mwanukuzi amewataka wakuu wa idara katika Wilaya hiyo kutatua kero za wananchi. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea)
Mwanukuzi ametoa maagizi hayo leo tarehe 17 Agosti, 2022 katika ziara ya mta kwa mta katika kata ya Rwengela.
Mkuu amesema wakuu wa idara wanapaswa kusikiliza wananchi ili kuzimaliza kwa wakati.
“Lengo la ziara hii ya mta kwa mta ni kusikiliza kero zenu naomba mziseme bila woga, na wakuu wa idara naomba mzifanyie kazi,” amesema.
Aidha, Mwanukuzi amewataka wakuu wa idara na viongozi wote kutoa elimu kuhusu umuhimu wa sensa, ili kumuunga mkono Rais Samia Suluhu Hassan.
Leave a comment