Tuesday , 3 October 2023
Home Habari Mchanganyiko Basi la Abood lapata ajali, dereva anusurika kifo
Habari Mchanganyiko

Basi la Abood lapata ajali, dereva anusurika kifo

Spread the love

DEREVA wa basi  la Abood lenye namba za usajili T 269 DBV ambaye jina lake halikufahamika mara moja amenusurika kifo baada ya kushambuliwa na wananchi wenye hasira, baada ya kugonga pikipiki aina ya Boxer. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Ajali hiyo imetokea maeneo ya Mbezi Kwa Msuguri baada ya gari hilo lililokuwa linafukuzana na basi lingine la BM katika barabara mpya na kuigonga pikipiki iliyokuwa inayokea njia ya pembeni na kuingia barabara kubwa.

Baada ya tukio hilo, dereva wa Abood alishuka kwa lengo la kuangalia kilichotokea, ndipo wananchi walipomvamia na kuanza kumshambulia, kabla ya kufanikiwa kukimbia na kurudi kwenye gari na kufunga milango.

Hali hiyo ilisababisha usumbufu kwa abiria ambao walikuwa wakitaharuki na kulazimika kutokea madirishani mpaka hapo walipofika polisi na kumuamuru dereva kufungua milango la kutoka nje.

Hakuna aliyefariki katika ajali hiyo, lakini mwanamke mmoja ambaye alikuwa abiria wa bodaboda (jina lake halikufahamika) alijeruhiwa kwenye mguu, kichwani na mkononi na amekimbizwa katika hospitali ya Bochi iliyopo Mbezi kwa Msuguri.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wawili wanaswa wakitengeneza noti bandia

Spread the loveJESHI la Polisi mkoani Songwe limewakamata watu wawili kwa tuhuza...

AfyaHabari Mchanganyiko

Chanjo mpya ya malaria Sh 5,000-10,000

Spread the loveShirika la afya la Duniani (WHO) limeridhia chanjo ya pili...

AfyaHabari Mchanganyiko

Wagonjwa kiharusi waongezeka, Hospitali Mkapa yaja matibabu mapya

Spread the loveHOSPITALI ya Benjamini Mkapa kwa kushirikiana na madaktari Bingwa kutoka...

Habari Mchanganyiko

Wananchi waamua kujenga zahanati kukwepa adha kufuata huduma mbali

Spread the loveWANANCHI wa Kijiji cha Kwikerege, kilichopo katika Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!