BASI la Kampuni ya Kilimanjaro linalofanya safari kutoka Tunduma kwenda Dar es Salaam asubuhi ya leo Jumatatu tarehe 14 Machi 2022, limepata ajali maeneo ya Senjele mkoani Songwe likiwa safarini kwenda jijini Dar es Salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu, Songwe … (endelea).
Katika picha ambazo zimesambaa mitandaoni zinaonesha basi hilo likiwa limeanguka na matairi yakiwa juu na abiria wanahangaika kutoka ndani ya basi hilo.
Haijafahamika kama kuna vifo ama majeruhi waliotokana na ajali hiyo.
Endelea kufuatilia MwanaHALISI TV na MwanaHALISI Online kwa habari na taarifa mbalimbali
Leave a comment