Tuesday , 30 May 2023
Habari za Siasa

Bashe apongezwa

Innocent Bashungwa, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
Spread the love

WAZIRI wa Viwanda na Biashara, Innocent Bashungwa amempongeza Naibu Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe kwa kiteuliwa kushika nafasi hiyo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Bashe aliteuliwa na Rais John Magufuli tarehe 21 Julai 2019, akichukua nafasi ya Bashungwa ambaye kwa sasa ameteuliwa kuwa Waziri wa Viwanda na Biashara.

Akizungunza na Waandshi wa Habari leo tarehe 23 Julai 2019 jijini Dar es Salaam, Bashungwa amesema, Rais Magufuli amefanya uteuzi sahihi kwa kuwaweka yeye na Bashe katika nafasi zinazotegemeana kwa majukumu.

Amesema, Watanzania wategemee makubwa kupitia ushirikiano baina ya wizara hizo mbili.

“Nitumie nafasi hii kumpongeza Hussein Bashe kwa kuaminiwa na rais, ameenda Wizara ya Kilimo kujazia nafasi yangu na katika kikao ambacho nimekutana na watu wa Holland, Waziri alimtuma Bashe kuwakilisha katika kikao hicho, Wizara ya Kilimo na Wizara ya Biashara Rais ametupanga vizuri,” amesema.

Katika hatua nyingine, Bashungwa amezungumzia mkutano wa 39 wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC).

Amesema, unatajiwa kufanyika Agosti mwaka huu, na kwamba jitihada za Rais Magufuli za kuiongoza Tanzania kuwa ya viwanda, ndio zimechangia kufuatia Tanzania kuchaguliwa kuwa mwenyeji wa mkutano huo.

“Tanzania ni sehemu ya SADC lakini upekee wetu ni kwamba sisi ni nchi ina amani, imejaliwa rasilimali na bandari. Ni fursa kwetu ukilinganisha na nchi zingine za SADC, fursa hii ni kubwa na tuitumie,” amesema.

Mkutano huo wa SADC utakaofanyika Agosti mwaka huu, utajumuisha mataifa 16 yanayounda jumuiya hiyo huku Rais Magufuli akichukua kiti cha Uenyekiti kutoka kwa Rais wa Namibia, Hage Geingog. Mkutano wa SADC mara ya mwisho nicni Tanzania ulifanyika mwaka 2003/2004 ambapo rais wa wakati huo, Benjamin Mkapa alichaguliwa kuwa mwenyekiti.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Uamuzi juu ya wakurugenzi kusimamia uchaguzi 13 Juni

Spread the love  MAHAKAMA ya Afrika ya Haki za Binadamu (ACHPR), imepanga...

Habari za Siasa

Musoma Vijijini waomba ujenzi wa barabara uanze haraka

Spread the loveJIMBO la Musoma Vijijini, mkoani Mara, limeomba Serikali kuhakikisha ujenzi...

Habari za Siasa

ACT Wazalendo yaanika madudu miradi ya ujenzi, moundombinu

Spread the loveCHAMA cha ACT Wazalendo kimeeleza wasiwasi juu ya uelekeo wa...

Habari za Siasa

Samia ashuhudia utiaji saini ujenzi wa minara 758 ya bilioni 265

Spread the love  RAIS Samia Suluhu Hassan ametoa wito kwa kampuni za...

error: Content is protected !!