Tuesday , 30 May 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Bashange ampigia chapuo Kubenea Kinondoni
Habari za Siasa

Bashange ampigia chapuo Kubenea Kinondoni

Spread the love

JORAN Bashange, Naibu Katibu Mkuu Bara wa Chama cha ACT-Wazalendo, amewataka wananchi wa jimbo la Kinondoni jijini Dar es Salaam pamoja na Kata ya Mzimuni kumpigia kura Saed Kubenea Mgombea Ubunge wa Jimbo hilo kupitia chama hicho. Anaripoti Faki Sosi, Dar es Salaam … (endelea).

Bashange ameyasema hayo jana Jumapili tarehe 20 Septemba 2020, alipokuwa akifungua mkutano wa kampeni za mgombea udiwani Kata ya Mzimuni, Kinondoni jijini Dar es Salaam, Bakar Kasubi.

Bashange amesema, wanakinondoni haihitaji mbunge atakayekubali kununuliwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kwamba kinamhitaji Kubenea aliyejitolea kupambana kwa ajili ya wananchi.

“Tunahitaji mbunge makini wa jimbo hili, hatuhitaji mbunge ambaye kuchaguliwa kwako sio kwa ajili ya biashara, kuchaguliwa kwake kuwe kwa ajili ya wananchi, mkienda kwenye kupiga kura mpigieni Kubenea na Kubenea Kinondoni itamelemeta,” amesema Bashange.

Saed Kubenea

Amewaeleza wananchi wa Mzimuni kuwa Kubenea ni mwanasiasa mwaminifu mwenyekupenda haki na kwamba wananchi wanatakiwa kumchagua kwa ajili ya maendeleo yao.

Amesema kuwa wananchi hawapaswi kuirejesha madarakani  Serikali ya CCM kwa kuwa  imevunja Katiba kwa kuzuia mikutano ya kidemokrasia ilhali iliiapa kuilinda.

Katika Bunge la 11 lililomaliza muda wake, Kubenea alikuwa mbunge wa Ubungo, Dar es Salaam kupitia Chadema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Uamuzi juu ya wakurugenzi kusimamia uchaguzi 13 Juni

Spread the love  MAHAKAMA ya Afrika ya Haki za Binadamu (ACHPR), imepanga...

Habari za Siasa

Musoma Vijijini waomba ujenzi wa barabara uanze haraka

Spread the loveJIMBO la Musoma Vijijini, mkoani Mara, limeomba Serikali kuhakikisha ujenzi...

Habari za Siasa

ACT Wazalendo yaanika madudu miradi ya ujenzi, moundombinu

Spread the loveCHAMA cha ACT Wazalendo kimeeleza wasiwasi juu ya uelekeo wa...

Habari za Siasa

Samia ashuhudia utiaji saini ujenzi wa minara 758 ya bilioni 265

Spread the love  RAIS Samia Suluhu Hassan ametoa wito kwa kampuni za...

error: Content is protected !!