Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Bashange ampigia chapuo Kubenea Kinondoni
Habari za Siasa

Bashange ampigia chapuo Kubenea Kinondoni

Spread the love

JORAN Bashange, Naibu Katibu Mkuu Bara wa Chama cha ACT-Wazalendo, amewataka wananchi wa jimbo la Kinondoni jijini Dar es Salaam pamoja na Kata ya Mzimuni kumpigia kura Saed Kubenea Mgombea Ubunge wa Jimbo hilo kupitia chama hicho. Anaripoti Faki Sosi, Dar es Salaam … (endelea).

Bashange ameyasema hayo jana Jumapili tarehe 20 Septemba 2020, alipokuwa akifungua mkutano wa kampeni za mgombea udiwani Kata ya Mzimuni, Kinondoni jijini Dar es Salaam, Bakar Kasubi.

Bashange amesema, wanakinondoni haihitaji mbunge atakayekubali kununuliwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kwamba kinamhitaji Kubenea aliyejitolea kupambana kwa ajili ya wananchi.

“Tunahitaji mbunge makini wa jimbo hili, hatuhitaji mbunge ambaye kuchaguliwa kwako sio kwa ajili ya biashara, kuchaguliwa kwake kuwe kwa ajili ya wananchi, mkienda kwenye kupiga kura mpigieni Kubenea na Kubenea Kinondoni itamelemeta,” amesema Bashange.

Saed Kubenea

Amewaeleza wananchi wa Mzimuni kuwa Kubenea ni mwanasiasa mwaminifu mwenyekupenda haki na kwamba wananchi wanatakiwa kumchagua kwa ajili ya maendeleo yao.

Amesema kuwa wananchi hawapaswi kuirejesha madarakani  Serikali ya CCM kwa kuwa  imevunja Katiba kwa kuzuia mikutano ya kidemokrasia ilhali iliiapa kuilinda.

Katika Bunge la 11 lililomaliza muda wake, Kubenea alikuwa mbunge wa Ubungo, Dar es Salaam kupitia Chadema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

error: Content is protected !!