KATIKA kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani, Wafanyakazi Wanawake wa kampuni ya Barrick kutoka ofisi ya Dar es Salaam wametembelea hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Mwananyamala na kukabidhi vifaa mbalimbali vya kusaidia matibabu vilivyotolewana kampuni hiyo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Pia wafanyakazi hao wamepata fursa ya kutembelea wodi ya wazazi ya hospitali hiyo.
Akiongea na uongozi wa Hospitali hiyo leo Machi 7, 2023 Meneja Mawasiliano wa Barrick Nchini (Corporate Communications and Country Liasion Manager) Georgia Mutagahywa, amesema katika kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani mwaka huu, pamoja na kampuni kuwa na programu mbalimbali za ndani pia imeandaa programu za kusaidia jamii.
Amesema Barrick, imekuwa ikitoa kipaumbele kuunga mkono jitihada za Serikali katika kuboresha sekta ya afya nchini ambapo kupitia fedha za uwajibikaji kwa jamii imeweza kujenga vituo vya afya katika maeneo yanayozunguka migodi yake ya Bulyanhulu na North Mara.
Kwa upande wake, Katibu wa Afya wa Hospitali hiyo,Lilian Mwanga. ameishukuru Barrick kwa msaada huo sambamba na baadhi ya wafanyakazi wake kujitolea muda wao kutembelea hospitali na kutembelea wagonjwa walioalazwa hospitalini hapo ikiwemo Wanawake waliolazwa katika wodi ya wazazi..
Leave a comment