Friday , 29 September 2023
Home Kitengo Michezo Barcelona wazuia wachezaji wake kwenye tuzo za FIFA
Michezo

Barcelona wazuia wachezaji wake kwenye tuzo za FIFA

Tuzo ya FIFA
Spread the love

RAIS wa klabu ya Fc Barcelona Josep Maria Bartomeu ataongoza ujumbe wa klabu katika tafrija ya utoaji tuzo wa mchezaji bora wa FIFA, lakini wachezaji wa klabu hiyo waliopata mualiko kwenye sherehe hiyo hawataudhulia kutokana na timu kuwa katika maandalizi ya mchezo wake unaofuta siku ya Juma tano dhidi ya Athletic Club, anaandika Kelvin Mwaipungu.

Barcelona watacheza mchezo wa marudiano katika dimba la Camp Nou baada ya kupoteza mchezo wa kwanza kwa kukubali kipigo cha mabao 2-1 dhidi ya Athletic Club ugenini.    

Mchezaji pekee wa Fc Barcelona alikuwa kwenye kinyang’anyiro hicho ni Leonel Messi ambaye atachuana na Cristiano Ronaldo wa Real Madrid na Antoine Griezmann kutoka Atletico Madrid wote kutoka ligi kuu nchini Hispania.

Tuzo hizo hapo awali zilikuwa zinajulikana kama Ballon d’Or lakini toka kuingia madarakani kwa rais mpya wa Shirikisho hilo la Soka duniani Gianni Infantino alibadilisha utalatibu huo na tuzo hiyo ya Ballon d’ Or iliendelea kuwa tuzo inayojitegemea kama ilivyokuwa hapo awali na FIFA kuwa na tuzo zaze ambzo zinatambilika kama The Best Fifa Awards.

Ujumbe wa klabu ya Fc Barcelona utaongozwa na Rais wa klabu hiyo  Josep Maria Bartomeu, makamu wa rais Jordi Mestre, mkurugenzi Silvio Elías, Mkurugenzi Mtendaji Oscar Grau, Albert Soler (mkurugenzi wa michezo mtaalamu), Robert Fernández  na Raúl Sanllehí.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Meridianbet yaibukia Tandika, yafungua duka jipya

Spread the love BAADA ya kupita maeneo mbalimbali hatimae kampuni yaMeridianbet imeibukia...

BiasharaMichezo

Ukiwa na Meridianbet ni rahisi kuwa milionea

Spread the love  CARABAO Cup raundi ya 3 Uingereza inaendelea na mechi...

Michezo

Jezi ya Samatta iliyoifunga Liverpool kuuzwa Genk

Spread the love  KLABU ya KRC Genk ya nchini Ubelgiji imeamua kuanza...

BiasharaMichezo

Hii ndio historia ya El-Clasico, derby bora zaidi duniani

Spread the love  KILA nchi ina vilabu viwili hasimu na pinzani nje...

error: Content is protected !!