Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Baraza la usalama latoa taarifa kuhusu Burundi
Kimataifa

Baraza la usalama latoa taarifa kuhusu Burundi

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa (UN)
Spread the love

BARAZA la usalama la Umoja wa Mataifa (UN), limetoa taarifa juu ya hali ya kisiasa nchini Burundi , ikiwa ni moja kati ya hatua zake za kulinda na kudumisha amani katika nchi za Africa, anaadika Catherine Kayombo.

Katika taarifa iliyosomwa na mwenyekiti wa baraza hilo, balozi Amr Abdellatif wa misri amebainisha kwamba hali ya kisiasa tete na hivyo kuongeza wakimbizi, mateso, mauaji ya kinyama na kutoweka kwa watu kadhaa.

Mwenyekiti huyo amesema baraza linasikitishwa na vitendo hivyo na kulaani vikali matamko katika umma.

Baraza hilo pia limekaribisha jitihada za nchi zinazoendelea ikiwamo kupokea wakimbizi kutoka Burundi.

Mgogoro wa kisiasa nchini Burundi umesababisha vifo vya watu zaidi ya 1,000 kwa mujibu wa mashirika ya haki za binadam na maelfu wengine kukimbilia nje ya nchi.

Mpaka sasa serikali ya Burundi haijaeleza lolote kuhusiana na ripoti ya baraza hilo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the loveZaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na...

Habari MchanganyikoKimataifa

Mgombea upinzani aongoza uchaguzi wa Rais Senegal

Spread the loveMgombea wa upinzani nchini Senegal, Bassirou Diomaye Faye ameonekana kuongoza...

error: Content is protected !!