Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Barakoa zatawala mkutano Rais Samia, wazee Dar
Habari MchanganyikoTangulizi

Barakoa zatawala mkutano Rais Samia, wazee Dar

Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amekwisha kuwasili ukumbi wa Mliman City, Dar es Salaam, ambapo atazungumza na wazee wa mkoa huo. Anaripoti Nasra Bakari, DMC … (endelea).

Mkutano huo na wazee, unafanyika leo Ijumaa, tarehe 7 Mei 2021.

Zaidi ya wazee 900 wamejitokeza kwenye ukumbi huo pamoja na viongozi mbalimbali akiwemo, Makamu wa Rais wa Tanzania, Dk. Philip Mpango, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan

Viongozi wote akiwemo Rais Samia, wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama na wazee, wamechukua tahadhari ya maambukizi ya virusi vya corona (COVID-19), kwa kuvaa barakoa.

Hii ni mara ya kwanza kwa shughuli kubwa kama hiyo kufanyika na kushuhudia wakiwa wamevalia barakoa.

Endelea kufuatilia MwanaHALISI Online, MwanaHALISI TV na mitandao yetu ya kijamii kwa habari na taarifa mbalimbali.

1 Comment

  • Sasa tumekubali kuvaa barakoa. Hoyeeee. Huu ni mwanzo mzuri. Tunategemea tutafuata maagizo mengine yote ya wataalamu.
    Ni tofauti na usemi wa JPM aliyedai kuwa eti damu ya Yesu inatulinda na akamshambulia Askofu aliyepingana naye
    Chama cha madaktari na Bakwata nao waliogopa kupingana naye. Sasa wabadilike. Pia na yale makanisa yanayodai kuponya Corona yabadilike. Waache kuwadanganya waumini !!!!

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Puma Energy Tz: Watanzania tudumishe amani kuvutia uwekezaji

Spread the loveKAMPUNI ya Mafuta ya Puma Tanzania imewakutanisha wadau mbalimbali katika...

Habari Mchanganyiko

DAWASA waanza utekelezaji agizo la Samia

Spread the loveMamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam...

Habari MchanganyikoKimataifa

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the loveTUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais wa...

KimataifaTangulizi

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the love  TUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais...

error: Content is protected !!