RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amekwisha kuwasili ukumbi wa Mliman City, Dar es Salaam, ambapo atazungumza na wazee wa mkoa huo. Anaripoti Nasra Bakari, DMC … (endelea).
Mkutano huo na wazee, unafanyika leo Ijumaa, tarehe 7 Mei 2021.
Zaidi ya wazee 900 wamejitokeza kwenye ukumbi huo pamoja na viongozi mbalimbali akiwemo, Makamu wa Rais wa Tanzania, Dk. Philip Mpango, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.

Viongozi wote akiwemo Rais Samia, wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama na wazee, wamechukua tahadhari ya maambukizi ya virusi vya corona (COVID-19), kwa kuvaa barakoa.
Hii ni mara ya kwanza kwa shughuli kubwa kama hiyo kufanyika na kushuhudia wakiwa wamevalia barakoa.
Endelea kufuatilia MwanaHALISI Online, MwanaHALISI TV na mitandao yetu ya kijamii kwa habari na taarifa mbalimbali.
Sasa tumekubali kuvaa barakoa. Hoyeeee. Huu ni mwanzo mzuri. Tunategemea tutafuata maagizo mengine yote ya wataalamu.
Ni tofauti na usemi wa JPM aliyedai kuwa eti damu ya Yesu inatulinda na akamshambulia Askofu aliyepingana naye
Chama cha madaktari na Bakwata nao waliogopa kupingana naye. Sasa wabadilike. Pia na yale makanisa yanayodai kuponya Corona yabadilike. Waache kuwadanganya waumini !!!!