KRZYSZTOF Buzalski, Balozi wa Poland nchini Tanzania ameungana na wadau wa masuala ya usafi, kusafisha ufukwe wa Kawe jijini Dar es Dalaam. Anaripoti Brightness Boaz, Dar es Salaam … (endelea).
Usafi huo umefanyika leo Jumatatu tarehe 21 Septemba 2020.
Mara baada ya kukamilisha shughuli hiyo, Balozi Buzalski amesema, amefurahishwa kushirikiana na Watanzania waliojitokeza kufanya usafi kwa sababu tatizo likitokea la uharibifu wa mazingira litaathiri watu wote.
Amesema, suala la taka za plastiki zipo kila sehemu na anafurahi kuona kila mwaka watu wakijitokeza kufanya usafi hivyo kila mmoja asimame katika nafasi yake kuzuia uchafuzi katika fukwe.
“Nimefurahi kuona Watanzania na wageni ambao wamejitokeza kufanya usafi kwa pamoja, kwa sababu tatizo tunalo kumbana nalo linaenda kutuadhiri wote, haijalishi unaishi Ulaya, Tanzania au Australia.”
“Uchafu wa plastiki upo kila mahali, kwa hiyo ninafuraha kila mwaka kuna kundi dogo la watu wanaoamu kuchukua nafasi katika shughuli ya usafi,” amesema Balozi Buzalski
Leave a comment