Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Tangulizi Balozi nne zakiuka taratibu, zalipa milioni 239
Tangulizi

Balozi nne zakiuka taratibu, zalipa milioni 239

Charles Kichere, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG)
Spread the love

 

MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) nchini Tanzania, Charles Kichere amebaini balozi nne zilifanya malipo yenye thamani ya Sh.239.56 milioni zaidi ya bajeti iliyoidhinishwa na bila ushahidi wa kibali cha kuhamisha fedha. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Katika ripoti yake inayoishia tarehe 30 Juni 2021 ambayo jana Jumanne 12 Aprili 2022 ameiwasilisha bungeni jijini Dodoma, CAG Kichere amesema “malipo kinyume na bajeti huathiri utekelezaji wa shughuli zilizopangwa, na hivyo kupelekea kutofikiwa kwa malengo yaliyokusudiwa.”

CAG amesema, “ninapendekeza menejimenti ya balozi husika kuhakikisha kuwa matumizi yote yanazingatia bajeti iliyoidhinishwa kama inavyoelekezwa kwenye Sheria ya Bajeti.”

Amezitaja balozi hizo na kiwango cha malipo ilichokifanya ni, Ubalozi wa Tananzania mjini Doha Sh.74.4 milioni, Ubalozi wa Tanzania- The Hugue Sh.45.4 milioni, Ubalozi wa Tanzania- Brussels Sh.5.3 milioni na Ubalozi wa Tanzania- Moroni Sh.114.3 milioni.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za SiasaTangulizi

Shibuda amlima waraka mzito Bulembo

Spread the loveMKONGWE wa siasa nchini, John Shibuda amemshukia kada maarufu wa...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

error: Content is protected !!