Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Balozi Ndobho afariki dunia
Habari Mchanganyiko

Balozi Ndobho afariki dunia

Spread the love

BALOZI Paul Ndobho, aliyewahi kuwa Mbunge wa Musoma vijijini kupitia NCCR-Mageuzi, amefariki dunia katika Hospitali ya Bugando, jijini Mwanza. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo tarehe 9 Septemba 2019 na Profesa Sospeter Muhongo, mbunge wa sasa wa jimbo hilo.

Taarifa ya Prof. Muhongo inaeleza kuwa, Balozi Ndobho amefariki dunia jana tarehe 8 Septemba 2019 saa 2 usiku.

“Aliyepata kuwa Mbunge wa Musoma Vijijini (NCCR-Mageuzi), Balozi Ndobho, amefariki dunia. Balozi Ndobho amekutwa na mauti jana Jumapili, 08.09.2019, saa 2 usiku akiwa kwenye matibabu kwenye Hospitali ya Bugando, jijini Mwanza,” imeeleza taarifa hiyo na kuwa taratibu za mazishi zinaendelea.

Balozi Ndobho alikuwa Mbunge wa Musoma Kaskazini mwaka 1965, na Musoma Vijijini mwaka 1995. Pia aliwahi kuwa Katibu wa Chama cha TANU, Mkoa wa Kigoma mwaka 1970.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

error: Content is protected !!