NAIBU Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk leo tarehe 5 Mei, 2022 amempokea Katibu Mkuu Jumuiya ya Madola, Patricia Scotland alipowasili Zanzibar katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Scotland yupo nchini kwa ziara maalumu ya kukutana na kumfahamisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan maudhui ya Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Madola unaotarajiwa kufanyika nchini Rwanda mwezi Juni 2022.
Leave a comment