Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Balozi Kanza aanza kuita wawekezaji kutoka Mexico, Marekani
Habari Mchanganyiko

Balozi Kanza aanza kuita wawekezaji kutoka Mexico, Marekani

Spread the love

Balozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico, Elsie Kanza amekutana kwa mazungumzo  na Meya wa mji wa Dallas, Meya Eric Johsnon pamoja na kufanya mazungumzo na Jumuiya ya Watanzania (Diaspora) waishio Marekani na Mexico. Anaripoti Mwandishi Wetu… (endelea)

Mazungumzo kati ya Balozi Kanza na Meya Eric Johnson yalilenga katika kuimarisha uchumi wa kidiplomasia hususan katika sekta za utalii, biashara na uwekezaji.

Balozi huyo amemuomba Meya Eric kuwahamasisha wafanyabiashara na wawekezaji kuja Tanzania kuwekeza kutokana na uwepo wa fursa nyingi huku mazingira ya biashara na uwekezaji yakiwa yameboreshwa kwa kuondoa kodi kero tangu serikali ya awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan uingie madarakani.

Katika mkutano na Watanzania waishio Marekani na Mexico amezungumzia juu ya namna ya kutangaza fursa mbalimbali za biashara na uwekezaji zilizopo Tanzania pamoja na kuweka mikakati ya kuwavutia watalii wengi kwenda Tanzania kutembelea vivutio mbalimbali vya uwekezaji.

Pia Balozi Kanza amefanya mazungumzo na Watanzania (diaspora) waishio Marekani katika Majiji ya Texas na Houston kwa lengo la kujitambulisha katika jumuiya hiyo na kujadiliana masuala mtambuka kuhusu maendeleo ya Tanzania.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!