Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Balozi John Kijazi afariki dunia
Habari za SiasaTangulizi

Balozi John Kijazi afariki dunia

Balozi John Kijazi
Spread the love

 

KATIBU Mkuu Kiongozi wa Serikali ya Tanzania, Balozi John Kijazi, amefariki dunia katika Hospitali ya Benjamin Mkapa, jijini Dodoma. Anaripoti Hamis Mguta, Dar es Salaam … (endelea). 

Taarifa ya Gerson Msigwa, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, imemnukuu Rais Magufuli akitangaza kifo hicho, kilichotokea leo Jumatano saa 3:10 usiku, tarehe 17 Februari 2021.

Msigwa amesema, taratibu za mazishi ya Balozi Kijazi zitatangazwa baadaye. Mungu amuweke mahali pema peponi, Amina.

Balozi Kijazi aliteuliwa na Rais Magufuli tarehe 6 Machi 2016 kuwa Katibu Mkuu Kiongozi, akichukua nafasi ya Balozi Ombeni Sefue. Kesho yake yaani 7 Machi 2016 akaapishwa, kuanza majukumu hayo.

Balozi Kijazi amewahi kuwa mwakilishi wa Tanzania nchini India, Singapore, Sri Lanka, Bangladesh na Nepal na pia ana makazi yake jijini New Delhi, India kuanzia mwaka 2007 na hivyo kumfanya kuwa Mkuu wa Mabalozi wote wanaowakilisha Tanzania nje ya nchi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari za SiasaTangulizi

CAG aibua madudu halmashauri 10, TANESCO na MSD

Spread the loveRIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali...

Habari za Siasa

Alichokisema Rais Samia baada ya kupokea ripoti ya CAG, TAKUKURU

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Serikali yake itafanyia kazi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

error: Content is protected !!