Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Bakwata yaitisha dua kudhibiti Korona, yahimiza barakoa ibadani
Habari Mchanganyiko

Bakwata yaitisha dua kudhibiti Korona, yahimiza barakoa ibadani

Katibu wa Baraza la Ulamaa la Bakwata, Sheikh Hassan Chizenga
Spread the love

 

BARAZA Kuu la Waislamu wa Tanzania (Bakwata), limewaagiza Maimamu wake kufanya dua maalumu wakati wa swala, ili Mungu aliepushe Taifa na janga la Ugonjwa wa Korona (UVIKO-19). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam …n(endelea).

Maelekezo hayo yametolewa leo Jumatano na Katibu wa Baraza la Ulamaa la Bakwata, Sheikh Hassan Chizenga, akizungumza na wanahabari mkoani Dar es Salaam.

“Baraza la Ulamaa linawaagiza Maimamu wote nchini, kufanya dua mbalimbali, pamoja na kusoma dua ya Kunuti katika kila swala, kumbembeleza Mola wetu alipeperushie mbali gonjwa hili,” amesema Sheikh Chizenga.

Mbali na kuitisha dua hiyo, Bakwata imetoa masharti kwa waumini wake, ili kukabiliana na maambukizi ya UVIKO-19, wakati wa ibada.

“Ibada ya Mungu ndiyo jambo muhimu kuliko yote ulimwenguni, kwa kuwa ndiyo kiunganishi baina ya mwanadamu na Mungu, hivyo havina budi kuendelea huku tukizingatia miko ya wizara ya afya, kama ilivyotolewa,” amesema Sheikh Chizenga.

Sheikh Chizenga ametaja masharti hayo ni, uwekaji vifaa vya kunawia mikono, ikiwemo maji safi yanayo tiririka na sabuni au vitakasa mikono.

Kila muumini kuvaa barakoa wakati wa ibada, pamoja na kukaa umbali wa mita moja kati ya mtu na mtu.

“Watu ambao kitaalamu wametambuliwa kuwa ni rahisi kuambukizwa gonjwa la UVIKO-19, kama wa kisukari, shinikizo la damu, kansa na kadhalika, wanashauriwa kujiweka mbali na mikusanyiko mikubwa ili kujilinda,” amesema Sheikh Chizenga.

2 Comments

  • Tunarudia yale yale. Ibada Ibada Ibada – Hayo yamepitwa na wakati Sheikh – Sasa ni wakati wa chanjo – Jitokezeni kumuunga mkono Mama !!!!!

  • Nawapongeza Mashekhe kwa uamzi mzuri kwani hakuna kinachoshindikana kwa Mungu. Asante sana..

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!