Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Bajeti 2021/22: Mabadiliko makubwa Jeshi la Polisi
Habari Mchanganyiko

Bajeti 2021/22: Mabadiliko makubwa Jeshi la Polisi

Simon Sirro, Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP)
Spread the love

 

WAZIRI wa Fedha na Mipango nchini Tanzania, Dk. Mwigulu Nchemba amesema, kuanzia mwaka wa fedha 2021/22, askari wa Jeshi la Polisi wataingia mkataba wa kipindi cha miaka sita na kuingia katika ajira ya kudumu. Anaripoti Jemima Samwel, DMC…(endele)

Dk. Mwigulu amesema hayo, leo Alhamisi, tarehe 10 Juni 2021, wakati akiwasilisha Bajeti ya Serikali kwa mwaka 2021/22, bungeni jijini Dodoma.

Amesema, katika jeshi la polisi kwa askari wapiganaji, kuna utaratibu wa wapiganaji kufanya kazi kwa mikataba ya muda mfupi kwa miaka 12 kabla hawajapata ajira za kudumu.

Dk. Mwigulu Nchemba, Waziri wa Fedha na Mipango

Amesema, jambo hili huwasababishia wapatapo mkataba wa kudumu wawe wamechelewa kwa miaka 12 ikilinganishwa na mtumishi mwingine aliyeingia pamoja kazini katika idara nyingine.

“Jambo hili linamadhara hasi katika itifaki ya utumishi na mafao ya mpiganaji anapostaafu. Hiki kimekuwa kilio cha muda mrefu cha askari wa Jeshi la Polisi,” amesema

Waziri huyo amesema, kutokana na changamoto hiyo, Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, “amesikia kilio cha askari hao na alituelekeza tukae na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi ili kutafuta suluhisho la jambo hili.”

Dk. Mwigulu amesema, “napendekeza kuanzia mwaka 2021/22 askari wa Jeshi la Polisi wataingia mkataba wa kipindi cha miaka 6 na kuingia katika ajira ya kudumu.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Gardner Habash wa Clouds Fm afariki dunia

Spread the loveALIYEKUWA mtangazaji wa kipindi cha Jahazi kinachorushwa na kituo cha...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

error: Content is protected !!