Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Bajeti 2021/22 kuzipa pumzi NGO’s
Habari Mchanganyiko

Bajeti 2021/22 kuzipa pumzi NGO’s

Spread the love

 

BAJETI Kuu pendekezwa ya Serikali ya Tanzania, kwa mwaka wa fedha wa 2021/22, imekuja na mikakati ya kuzipa nafuu Taasisi Zisizo za Kiserikali (NGO’s), ikiwemo kusamehe kodi ya ongezeko la thamani (VAT), kwenye bidhaa na huduma za miradi inazotekeleza. Anaripoti Nasra Bakari, DMC…(endelea).

Hyao yamesemwa leo Alhamisi, tarehe 10 Juni 2021 na Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Mwigulu Nchemba, akiwasilisha mapendekezo ya Bajeti Kuu ya Serikali kwa 2021/22, bungeni jijini Dodoma.

“Napendekeza Kutoa msamaha wa kodi ya ongezeko la thamani, kwa NGO’s, kwenye bidhaa na huduma zitakazotumika kwenye miradi inayotekelezwa na taasisi husika,”

“Aidha, taasisi zitakazonufaika na msamaha huo, ni zile ambazo zina mikataba na Serikali, yenye kipengele kinachotoa msamaha wa kodi ya ongezeko la thamani,” amesema Dk. Mwigulu.

Dk. Mwigulu Nchemba, Waziri wa Fedha na Mipango

Dk. Mwigulu amesema hatua hiyo inalenga kupunguza ukiritimba katika upokeaji wa fedha za misaada za miradi ya maendeleo.

“Kumekwepo na ukiritimba katika kupokea fedha za misaada, kwenye miradi ya maendeleo kwa hitaji la kisheria la kusubiri idhini ya Baraza la Mawaziri likae ili kuidhinisha misamaha,” amesema Dk. Mwigulu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Gardner Habash wa Clouds Fm afariki dunia

Spread the loveALIYEKUWA mtangazaji wa kipindi cha Jahazi kinachorushwa na kituo cha...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

error: Content is protected !!