Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Bajeti 2021/22 kupitishwa? Spika Ndugai atoa onyo
Habari Mchanganyiko

Bajeti 2021/22 kupitishwa? Spika Ndugai atoa onyo

Job Ndugai Spika wa Bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania
Spread the love

Bajeti 2021/22 kupitishwa? Spika Ndugai atoa onyoMJADALA wa Bajeti ya Serikali ya Tanzania kwa mwaka 2021/22 ya Sh.36.3 Trilioni, unahitimishwa leo Jumanne, tarehe 22 Juni 2021, bungeni jijini Dodoma. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Tayari Spika wa Bunge, Job Ndugai ametoa onyo kwa mbunge ambaye hatopiga kura kuipitisha bajeti hiyo huku akiwa hana ruhusa yake, litakalomkuta “ni la kwakwe mwenyewe.”

Bajeti hiyo, iliwasilishwa bungeni hapo, Alhamisi tarehe 10 Juni 2021 na Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Mwigulu Nchemba.

Baada ya kuiwasilisha, wabunge walipata fursa ya kuijadili kuanzia tarehe 14 Juni 2021.

Dk. Mwigulu Nchemba, Waziri wa Fedha na Mipango

Leo Jumanne asubuhi, kabla ya kipindi cha maswali na majibu kuanza, Spika wa Bunge hilo, Job Ndugai amewashukuru wabunge kwa kuijadili vyema bajeti hiyo, ikiwemo wenyeviti wa Bunge na Naibu Spika, Dk. Tulia Ackson kwa kuongoza Bunge.

“Leo ni siku ya uamuzi na kwa mbunge ambaye hayupo hapa na hatapiga kura yake, hilo ni la kwake mwenyewe,” amesema Spika Ndugai

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

error: Content is protected !!