Tuesday , 19 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Bajeti 2021/2022: Wabunge 94% wasema ‘Ndiooo’
Habari za SiasaTangulizi

Bajeti 2021/2022: Wabunge 94% wasema ‘Ndiooo’

Spread the love

 

ASILIMIA 94 ya Wabunge wa Bunge la Jamhuri Tanzania, jijini Dodoma wamepitisha Bajeti Kuu ya serikali ya Sh. 36.3 Trilioni kwa mwaka wa fedha 2021/2022. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)

Bajeti hiyo imepitishwa leo Jumanne, tarehe 22 Juni 2021, baaada ya wabunge kupiga kura ya wazi, kufuatia kufungwa mjadala wa makadirio ya mapato na matumizi ya Serikali, kwa mwaka huo wa fedha.

Akitoa matokeo ya zoezi hilo, Spika Job Ndugai amesema,  wabunge 23 kati ya 385 waliohudhuria bungeni, wamepiga kura ya wasiokuwa na upande (Abstain) huku 361 wakipiga kura ya ndiyo.

Bunge la Tanzania

“Kura za hapana kwa mara ya kwanza hakuna hata moja, kura za ambao hawakuamua ni 23, yaani walio-Abstain ni 23.  Idadi ya wabunge wote waliokuwemo humu bungeni ilikuwa 385, wabunge waliokuwa hawapo watano, hivyo ambao hawakuamua ni asilimia 6,” amesema Spika Ndugai.

Spika Ndugai ameongeza “na waliokubali kupitisha bajeti hii ni 361 ambayo ni asilimia 94, asilimia hii ni kubwa kabisa  ambayo katika kumbukumbu za bunge miaka ya karibuni haijapata kutokea.”

Bajeti hiyo imepitishwa baada ya wabunge kuijadili kwa muda wa siku sita, tangu ilipowasilishwa bungeni na Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Mwigulu Nchemba, tarehe 10 Juni mwaka huu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Zanzibar mbioni kuanza uchimbaji mafuta na gesi baharini

Spread the loveSERIKALI ya Zanzibar, imekamilisha mchakato wa uchimbaji wa mafuta na...

Habari za Siasa

Wizara ya afya yataja mafanikio 10 miaka mitatu Samia madarakani

Spread the loveWIZARA ya Afya imetaja mafanikio 10 iliyoyapata ndani ya miaka...

Habari za Siasa

Mbozi walilia kuwa manispaa, majimbo 3

Spread the loveHALMASHAURI ya wilaya ya Mbozi mkoani Songwe imeeleza dhamira yake...

Habari za Siasa

Wabunge waitaka TPDC kuongeza kasi ya kuunganisha wateja gesi asilia

Spread the love  KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini...

error: Content is protected !!