Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Bajeti 2019/20: Ada leseni za udereva, usajili magari wapanda
Habari Mchanganyiko

Bajeti 2019/20: Ada leseni za udereva, usajili magari wapanda

Spread the love

SERIKALI ya Tanzania imependekeza kupanda kwa ada ya leseni ya udereva kutoka Sh. 40,000 za sasa, mpaka Sh. 70,000 kwa Mwaka wa Fedha 2019/20 unaoanzia Julai Mosi mwaka huu. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Akisoma Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/20 leo tarehe 13 Juni 2019 bungeni jijini Dodoma, Dk. Philip Mpango, Waziri wa Fedha na Mipango amesema, kupandisha ada huku kunakwenda sambamba na kuongeza uhai wa leseni hizo kutoka miaka mitatu mpaka mitano.

Pia Dk. Mpango ameeleza kuwa, serikali imependekeza kuongeza tozo za usajili wa magari kutoka Sh. 10,000 hadi Sh. 50,000, kwa pikipiki za matairi matatu (bajaji) kutoka Sh. 10,000 hadi Sh. 30,000 na pikipiki za kawaida kutoka Sh. 10,000 hadi Sh. 20,000.

Akieleza sababu za kuongeza muda wa utoaji leseni pamoja na kuongeza ada hiyo Dk. Mpango amesema, lengo ni kupunguza gharama za kuchapisha leseni mara kwa mara kwa kuwa, leseni hizo zinaweza kudumu hata zaidi ya miaka mitano.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

error: Content is protected !!