Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Bado siku mbili Trump ahamie Ikulu
Kimataifa

Bado siku mbili Trump ahamie Ikulu

Ikulu ya Marekani
Spread the love

RAIS mteule Donald Trump wa Marekani amebakisha muda usiozidi siku mbili kabla ya kuapishwa rasmi kuwa rais wa taifa hilo lenye nguvu kubwa ya kiuchumi duniani, anaandika Wolfram Mwalongo.

Trump anatarajia kuapishwa Ijumaa ya wiki hii (tarehe 20 Januari), tayari kuiongoza Marekani ingawa takwimu za mtandao wa habari wa NBC zinaonesha kuwa ni asilimia 44 tu ya Wamarekani wanaoafiki ushindi wake.

Takwimu za NBC zinashabihiana na ushindi wa Trump wa asilimia 46 alioupata katika uchaguzi mkuu wa tarehe 8 Novemba mwaka jana.

Ijumaa ya wiki hii Trump anatarajia kuhamishia rasmi makazi yake katika Ikulu ya White House huku Barack Obama akitarajia kufungasha kila kilicho chake.

Wakati takwimu za NBC zikionesha kuwa Wamarekani wana imani na Trump kwa asilimia 44 tu, mtangulizi wake Barack Obama katika kipindi kama hiki mwaka 2009 aliingia Ikulu huku akiungwa mkono kwa asilimia 71.

George Bush Rais wa 43 aliingia Ikulu mwaka 2001akikubalika kwa silimia 57 huku Bill Clinton mwaka 1991akiwa na asilimia 77.

Wachambuzi wa masuala ya siasa za Magharibi wamesema huenda wapinzani wa Trump wakatumia mwanya huo kuzorotesha uongozi wake kama njia ya kumwangusha katika uchaguzi unaofuata.

Hata hivyo bilionea huyo anaonekana kutojali maneno yanayozungumzwa huku akisema yupo tayari kurejesha hadhi ya taifa hilo.

Mpaka sasa ameendelea kupiga vita jumuiya za kimataifa anazoamini taifa lake linachangia kiasi kikubwa cha fedha katika mambo yasiyo na maslahi kwa Marekani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!