Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari Baba mzazi wa DED Kiteto, Balozi Nchimbi afariki dunia
Habari

Baba mzazi wa DED Kiteto, Balozi Nchimbi afariki dunia

Spread the love

 

JOHN Alphoso Nchimbi, baba mzazi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kiteto (DED), Mkoa wa Manyara, John Nchimbi amefariki dunia, katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI). Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Mzee Nchimbi ambaye ni mwanasiasa mkongwe nchini na mwanachama wa Chama Cha mapinduzi (CCM), amefikwa na mauti usiku wa kumakia leo Jumapili, Taasisi ya Jakaya Kikwete (JKCI), jijini Dar es Salaam.

John amesema, “kwa huzuni kubwa sana, Leo nimempoteza my mentor, my hero, my love, my protector my everything aliyenipenda sana, aliyenitunza na kunilea, baba yangu mzazi.”

Aidha, Mzee Nchimbi ni baba mzazi wa aliyewahi kuwa waziri wa mambo ya ndani wa Tanzania, Balozi Emmanuel Nchimbi.

Msiba upo nyumbani kwa Mzee Nchimbi, Tabata Relini jijini Dar es Salaam ambapo taratibu za mazishi zinafanyika.

Endelea kufuatilia MwanaHALISI TV, MwanaHALISI Online na mitandao yetu kwa habari na taarifa mbalimbali

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

HabariSiasa

Dk. Rose Rwakatare atoa kadi 500 kila Wilaya Morogoro

Spread the loveMWENYEKITI wa Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Morogoro, Dk...

ElimuHabari

CBE, WMA wasaini makubaliano wanafunzi kusoma wakifanyakazi

Spread the loveNAIBU Spika Musa Azzan Zungu amekipongeza Chuo cha Elimu ya...

HabariTangulizi

Dk. Slaa, Mwabukusi kuhojiwa na jeshi la Polisi Mbeya

Spread the loveJESHI la Polisi jijini Mbeya, linawashikilia kwa mahojiano Dk. Wilbroad...

HabariHabari Mchanganyiko

Kairuki Hospital Green IVF  yawanoa madaktari kuhusu upandikizaji mimba

Spread the love KITUO cha Upandikizaji Mimba cha Kairuki Hospital Green IVF...

error: Content is protected !!