Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Baba mbaroni kwa kufyeka ‘matiti’ ya binti’ye kwa jiwe la moto
Kimataifa

Baba mbaroni kwa kufyeka ‘matiti’ ya binti’ye kwa jiwe la moto

Spread the love

 

POLISI wa jimbo la Lagos nchini Nigeria wamemtia mbaroni mwanaume mmoja kwa madai ya kuyaondoa matiti ya binti yake mwenye umri wa miaka nane kwa kutumia jiwe la moto. Anaripoti Helena Mkonyi, TUDARCo … (endelea).

Baba huyo aliyefahamika kwa jina la Banjo Adegboyega anadaiwa kutekeleza unyama huo ili kuzuia chuchu za binti yake zilizokuwa zimeanza kukua kutokana na mabadiliko ya mwili.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo, Msemaji wa polisi wa jimbo hilo, DSP Asijebotu amesema wanamshikilia mwanaume huyo ambaye pia ni Mhandisi ili kurahisisha uchunguzi kuhusu tukio hilo.

Amesema kwa sasa msichana huyo amelazwa hospitalini kwa matibabu, huku ripoti zikisema kuwa yuko mahtuti kutokana na majeraha aliyosababishiwa na baba yake mzazi.

Aidha, taarifa za Baba huyo kutekeleza ukatili huo ziliripotiwa polisi na Mtandao wa Kikundi cha wanaharakati wa kutetea haki za watoto.

Mkuu wa mtandao huo, Ebenezer Omejalile amewaeleza waandishi wa habari kuwa mwanaume huyo aliyefahamika kwa jina la Panel, “aliyabana na kisha kuyachoma matiti ya binti yake.

“Baba wa msichana huyo alitumia jiwe la moto alilolifunga ndani ya nguo na kumchoma hadi alipohakikisha kuwa ameyaharibu kabisa matiti ya binti yake,” alisema.

Alisema pia kwamba baba huyo alielezea kutoridhishwa kwake na jinsi binti yake alivyokuwa ameanza kuonyesha dalili za saratani ya matiti kwenye matiti yake ndio maana alitaka kuyazuia yasiote.

“Jambo la kushangaza ni jinsi baba huyo alivyosema amekuwa akimuogesha binti yake wa miaka 8 kila siku,” amesema.

Mama yake msichana huyo alisema Banjo amekuwa akimpiga binti yake mara kwa mara.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!