Wednesday , 29 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Baba aua familia yake kwa kutumia jembe
Habari Mchanganyiko

Baba aua familia yake kwa kutumia jembe

Spread the love

AMMY    Lukule ambaye ni mhasibu katika Hospitali ya Rufaa ya Mbeya amefanya mauji kwa familia yake kutokana na wivu wa mapenzi, Anaripoti Hamis Mguta.. (endelea).

Lukule  amefanya tukio hilo usiku wa kuamkia jana na kisha kutimkia pasipojulikana.
Kaimu Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Benedict Kitalika amethibitisha kutokea kwa mauaji hayo na

kusema kuwa muuaji alifanya tukio hilo usiku wa kuamkia jana nyumbani kwake eneo la Kimara jijini Dar es Salaam na kisha kutokomea kusikojulikana.

“Ni kweli mwanaume mmoja ambaye anafanya kazi ya uhasibu katika hospitali ya rufaa ya Mbeya, aliyejulikana kwa jina la Ammy Lucas Lukule, ameua mke, mtoto na shemeji yake, inasemekana kulikuwa na ugomvi ambapo mwanaume alikuwa akimtuhumu mkewe kuwa mtoto mdogo siyo wake na anajihusisha na mapenzi na wanaume wengine, hivyo aliamua kuwaua kwa jembe na kukimbia”, amesema Kamanda Kitalika.

Kamanda Kitalika amesema kuwa baada ya kufanya tukio hilo mtuhumiwa huyo  aliacha ujumbe kuwa polisi wasihangaike kwani yeye ndiye kafanya mauaji hayo.

Jeshi la Polisi limesema taarifa za tukio hilo walizipata kutoka kwa majirani baada ya kugundua hakuna dalili ya kuwepo watu kwenye hiyo nyumba na kuanza kuchunguza, ndipo walipogundua hayo na kuita polisi kuvuja mlango.

Kamanda Kitalika amesema jeshi la polisi linaendelea kufanya uchunguzi wake kubaini alipo mhusika na kumchukulia hatua za kisheria.

Waliouawa wametajwa kuwa ni Upendo Lukule ambaye ndiye mke, Magreth Samuel ambaye ni shemeji yake na mtoto mdogo mwenye chini ya mwaka mmoja.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Rais Samia awataka wahariri kufanya kazi bila uoga, upendeleo

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan amewataka wahariri wa vyombo...

Habari Mchanganyiko

STAMICO yasaini mkataba wa bilioni 55.2 kuchoronga miamba GGML

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limezidi kufanya vizuri katika...

Habari Mchanganyiko

NMB yatoa traksuti za Mwenge wa Uhuru Mtwara

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa traksuti kwa mkoa wa Mtwara ambako...

Habari Mchanganyiko

Yara yaja na bima ya mazao kwa wakulima

Spread the love  WAKATI serikali ikiweka mikakati mbalimbali kuimarisha sekta ya kilimo...

error: Content is protected !!