Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Baba amuua bintiye, kisa kujiozesha
Kimataifa

Baba amuua bintiye, kisa kujiozesha

Romana Ashrafi, enzi za uhai wake
Spread the love

ROMANA Ashrafi (14), raia wa Iran, ameuawa kwa kushambuliwa kwa mundu na baba yake mzazi Reza Ashraf, kwasababu ‘alijiozesha.’ Nchini humo mauaji hayo yanaitwa ‘mauaji ya heshima.’ Inaripoti mitandao ya kimataifa … (endelea).

Kwa utamaduni wa Iran, ‘mauaji ya heshima’ ni mauaji ya ndugu wa familia ambaye anadaiwa kupeleka aibu miongoni mwa watu wa familia.

Taarifa zaidi nchini humo zinaeleza, binti huyo alitoroka nyumbani kwao na mpenzi wake, Bahamn Khavari (35) na kukimbilia mji wa Talesh baada ya baba yake kupinga wawili hao kufunga ndoa.

Siku tano baada ya Bahamn na Romana kutoroka, taarifa ziliwafikiwa polisi na kuanza kuwasaka wiki iliyopita.

Baada ya kupatikana kwao, Romana aliwaambia maofisa hao kwamba anahofia maisha yake pale ataporejesha kwa baba yake. Hata hivyo, ‘alipuuzwa.’

Baada ya kurejeshwa nyumbani, kwa hasira baba yake alimkakataka kwa mundu na kisha kukiri kufanya hivyo.

Tayari Reza anashikiliwa na vyombo vya usalama vya taifa hilo, mauaji hayo yameibua hisia kali nchini humo na kutuhumu sheria kushindwa kuwalinda wanawake.

Sheria za nchi hiyo zinawapunguzia adhabu wazazi wanaofanya mauaji kwa jina la ‘mauaji ya heshima’ na adhabu yake kuwa kati ya miaka mitatu hadi 10.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!