Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Baadhi wakaidi kunawa mikono, kisa watu weusi hawapati corona
Habari Mchanganyiko

Baadhi wakaidi kunawa mikono, kisa watu weusi hawapati corona

Spread the love

PAMOJA na kutolewa kwa elimu juu ya kujikinga na virusi vinavyosababisha ugonjwa hatari duniani wa corona bado jamii imekuwa na fikra hasi kwa madai kuwa watu weusi hawawezi kukumbwa na ugonjwa huo. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Hali hiyo imebainishwa na Mariam Masenga, mmoja wa wasimamizi wa zoezi la kunawa mikono kwa wafanyabiashara na wateja katika soko la Bonanza, jijini Dodoma linalouza samaki, mbogamboga na matunda.

Mariam alisema kuwa anakumbana na changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na kukutana na baadhi ya watu ambao wanakuwa wabishi kunawa mikono kwa madai kuwa watu weusi hawapatwi na corona.

“Kunatakiwa elimu kubwa sana kwa jamii, changamoto iliyopi, kuna watu wanakataa kunawa, wakidai kuwa eti wananawa kwani kuna chakula? wengine wanasema eti corona haiwapati watu weusi, inatulazimu kuwalazimisha na wakigoma hawaruhusiwi kuingia sokoni.

“Sijui nani katoa elimu kuwa watu weusi hawawezi kupatwa na ugonjwa huu wa corona, serikali na wataalamu wa afya wanatakiwa kutoa elimu ya kutosha ili kuondosha upotoshaji huu,” alisema Mariam.

Naye Katibu  mkuu wa soko hilo, Dickson Mwesigwa alisema kuwa kutokana na kuwepo kwa ugonjwa huo ambao ni tishio kwa dunia uongozi wa soko umelazimika kuweka vifaa mbalimbali ikiwa ni pamoja na vitakatisha mikono katika milango miwili ya soko na kuwaweka wasimamizi ambao watahakikisha kila anayeingia sokoni hapo ananawa mikono.

Alisema kuwa vifaa hivyo ambavyo vimewekwa katika milango maalumu ya kuingilia katika soko hilo na kuwaweka wasimamizi ni wajibu wa kila mmoja kuhakikisha ananawa mikono pindi anapotaka kuingia ndani ya soko na bila kujali anayeingia sokoni ni mfanya biashara au ni mteja.

“Sokoni tunapokea watu wengi, huwezi kujua nani mwathirika na ni nani ambaye yupo salama kutokana na hali hiyo uongozi wa soko la bonanza ambalo ni maarufu kwa kuuza samaki, matunda na mbogamboga ,tumeamua kutekeleza kwa vitendo maagizo ya serikali na wataalamu wa afya kwa kuweka vifaa mbalimbali vya kujikinga na ugonjwa huo,” alisema Katibu Mwesigwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!