Saturday , 2 December 2023
Home Habari Mchanganyiko Baada ya siku 342 gerezani, DPP awafutia mashtaka bosi MSD, mwenzake
Habari MchanganyikoTangulizi

Baada ya siku 342 gerezani, DPP awafutia mashtaka bosi MSD, mwenzake

Aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Laurean Bwanakunu
Spread the love

 

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, imewaachia huru, aliyekuwa mkurugenzi mkuu wa Bohari ya Dawa (MSD), Laurean Bwanakunu na Mkurugenzi wa Logistiki, Byekwaso Tabura. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Wawili hao, wameachia huru leo Alhamisi, tarehe 13 Mei 2021, na Hakimu Mkazi Mwandamizi, Kassian Matembele.

Ni baada ya wakili wa serikali Mwandamizi, Wankyo Simon kuwasilisha hati ya kuwafutia mashtaka washtakiwa hao, iliyosainiwa na aliyekuwa DPP, Biswalo Mganga tarehe 10 Mei, 2021, akionesha kuwa hana nia ya kuendelea na mashtaka dhidi yao.

          Soma zaidi:-

Hadi wanaachiwa huru, wawili hao, wamekaa gerezani kwa siku 342 kuanzia tarehe 5 Juni 2020, walipofikishwa kwa mara ya kwanza mahakamani hapo, wakitokea Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru).

Katika kesi hiyo, washtakiwa hao walikuwa wakikabiliwa na mashtaka matano likiwemo utakatishaji fedha haramu zaidi ya Sh.1.6 bilioni.

Kwa mujibu wa hati ya mashtaka inadaiwa kati ya tarehe 1 Julai, 2016 na 30 Juni 2019, maeneo mbalimbali ya jiji na mkoa wa Dar es Salaam, wakiwa watumishi wa umma kwa pamoja walitengeneza genge la uhalifu kwa ajili ya kujipatia faida.

Pia, washtakiwa wote kwa pamoja wanadaiwa kuisababishia MSD hasara ya Sh.3.8 bilioni

Inadaiwa Bwanakunu akiwa ni mtumishi wa umma alifanya matumizi mabaya ya madaraka kwa kongeza mishahara na posho za wafanyakazi bila ruhusa ya Katibu Mkuu Utumishi na kuisababishia MSD hasara ya Sh Sh.85.1 milioni

Katika shtaka jingine, ilidaiwa kati ya tarehe 1 Julai 2016 na 30 June 2019, katika maeneo ya Keko Wilaya ya Temeke Mkoa wa Dar wa Salaam wote kwa pamoja walijipatia fedha Sh 1.6 bilioni wakijua fedha hizo ni zao la uhalifu ambao ni kuongoza genge la uhalifu.

Ni baada ya aliyekuwa DPP, Biswalo Mganga kutokuonesha nia ya kuendelea na kesi dhidi yao.

Biswalo kwa sasa ni Jaji wa Mahakama kuu ambaye aliteuliwa na Rais Samia Suluhu Hassan Tarehe 11 Mei 2021, anasubili kaupishwa yeye pamoja na wenzake 28

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari Mchanganyiko

GGML waungana na Biteko kuanika mbinu za mapambano dhidi ya Ukimwi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari MchanganyikoTangulizi

Mwalimu jela miaka mitatu kwa rushwa

Spread the loveMAHAKAMA ya Hakimu Mfawidhi, wilaya ya Igunga, mkoani Tabora imemhukumu...

Habari Mchanganyiko

Waziri Bashungwa aagiza wahandisi kujengewa uwezo

Spread the loveWAZIRI wa Ujenzi, Innocent Bashungwa ameiagiza Bodi ya Usajili wa...

Habari Mchanganyiko

Heche ataka mawakili vijana kuamka sakata Mpoki

Spread the loveMWENYEKITI wa Mawakili Vijana Tanzania kutoka Chama cha Mawakili wa...

error: Content is protected !!