Wednesday , 24 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Baada ya Segerea, Mbowe kuongoza Kamati Kuu leo
Habari za SiasaTangulizi

Baada ya Segerea, Mbowe kuongoza Kamati Kuu leo

Spread the love

FREEMAN Mbowe, Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)-Taifa, pamoja na wajumbe wa Kamati Kuu wanakutana leo tarehe 30 Machi 2019 kujali hali ya kisiasa nchini. Anaripoti Bupe Mwakiteleko…(endelea).

Taarifa iliyotolewa na Tumaini Makene, Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano ya chama hicho imeeleza kuwa, kikao hicho ni cha siku moja na kilichofanywa kwa mujibu wa Katiba ya Chadema toleo la mwaka 2016.

Kikao hicho kitaongozwa na Mbowe, ikiwa ni baada ya kukosa vikao kadhaa kutokana na kuwekwa rumande katika Gereza la Segerea tangu Novemba mwaka jana mpaka alipopata dhamana tarehe 7 Machi 2019.

Kazi zinazotarajiwa kufanywa na kamati hiyo ni pamoja na kupokea taarifa na kujadili mwenendo wa kisiasa nchini, na kisha kuchukua mwelekeo baada ya mjadala wa taarifa hiyo.

Kamati Kuu hiyo inakutana ikuwa ni baada ya siku nne viongozi wakuu wa vyama vya upinzani nchini, kukutana na kujadili mwenendo wa hali ya siasa nchini.

Mkutano viongozi hao wakuu uliitishwa baada ya Jeshi la Polisi kuzuia Mkutano wa Chama cha ACT-Wazalendo kwa madai kwamba, Chama cha Wananchi (CUF) kilipanga kufanya vurugu. Mkutano wa viongozi hao ulidumu kwa saa tatu.

Viongozi waliohudhuria mkutano huo uliofanyika katika Makao Makuu ya Chadema, Kinondoni jijini Dar es Salaam ni pamoja na Mbowe; Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Vincent Mashinji; Naibu Katibu Mkuu Zanzibar, Salum Mwalim; Kiongozi wa ACT,  Zitto Kabwe, Mwenyekiti wa ACT-Wazalendo, Yeremia Maganja pamoja na mwanachama mpya wa ACT-Wazalendo, Maalim Seif Shariff Hamad.

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

error: Content is protected !!