
Wachezaji wa Azam FC wakishangilia moja ya bao walilofungwa katika mchezo wao dhidi ya Mtibwa Sugar
MABINGWA watetezi, Azam FC wamefanikiwa kurejea kileleni katika msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara baada ya kuichakaza Mtibwa Sugar kwa mabao 5-2 katika mchezo uliochezwa kwenye Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam. Anaripoti Erasto Stanslaus …. (endelea).
Kwa ushindi huo, Azam FC imewaondoa kileleni Yanga kwa kufikisha pointi 25 baada ya kucheza mechi 13, sawasawa na Yanga lakini wamezidiwa wastani wa mabao.
Mabao ya Azam FC yalifungwa na Kipere Tchetche dakika 18 na 86, Frank Domayo dakika 26 na 58 na Didier Kavumbangu.
Mtibwa Sugar walipata mabao yao kupitia kwa Mussa Nampaka dakika ya 34 na Ame Ally aliyefungwa bao la pili dakika ya 70.
More Stories
Bumbuli huru, ashinda rufaa yake
Manchester United kuivaa AC Milani, 16 bora Europa
Poulsen awabakisha Mgunda, Matola Taifa Stars