Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Michezo Azam TV kufunga taa viwanja vinne, ligi kuu kupigwa usiku
Michezo

Azam TV kufunga taa viwanja vinne, ligi kuu kupigwa usiku

Uwanja wa Gwambina, uliopo Mwanza
Spread the love

 

KAMPUNI ya Azam Media, wamekuja na mradi wa kufunga taa kwenye viwanja vinne vinavyochezewa Ligi kuu Tanzania Bara. Anaripoti Kelvin Mwaipungu… (endelea)

Lengo la mpango huo ni, kuondoa mechi zaa saa 8 mchana ambazo zinawanyima watu wengi fursa za kutazama mpira kutokana na kuwa kwenye shughuli zao za kila siku.

Viwanja ambavyo vitakuwa sehemu ya mradi huo ni Uwanja wa Majaliwa ulipo Lindi unaotumia na Namungo FC na uwanja wa Kaitaba uliopo Kagera unaotumia na Kagera Sugar.

Vingine ni, Mkwakwani jijini Tanga unaotumia na Costal Union pamoja na Uwanja wa Gwambina ulipo Mwanza, unaotumiwa na Gwambina FC.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumanne tarehe 16 Februari 2021, kwenye makao makuu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), jijini Dar es Salaam, mwakilishi kutoka Azam Media, Mhandisi Ndozero amesema, mradi huo umezingatia sehemu nzuri ya kuchezea (Pitch) na mazingira yote ya uwanja.

“Tuna kila sababu ya kuhakikisha mradi huu unakwenda kama, sisi tumejitahidi kufuata utaratibu wote unahitajika, na lengo kubwa ni kuepukana na mechi saa 8 mchana kwa kuwa zinaumiza kwani kuna nyakati haziepukiki licha ya bodi ya Ligi kujitahidi,” amesema

“Michakato utakapo kamilika bodi ya Ligi watakuwa na nafasi ya kupanga mechi kuchezwa muda wote kuanzia saa 1 usiku na mantiki hiyo tutapata picha zilizo bora” amesema Ndozero

Aidha, Ndozero amesema, sababu za zimesababisha biashara zimesababisha kuamua kufunga taa kwenye viwanja hivyo ili watu wengi waliolipia ving’amuzi vyao waweze kutaza michezo mingi zaidi katika muda mzuri.

Amesema, toka kuanza kwa msimu huu Azam TV imeonesha idadi kubwa ya michezo ya Ligi Kuu Tanzania Bara na kufanya mechi nyingi kuonekana ukitofautisha katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!