Friday , 29 September 2023
Home Kitengo Michezo Azam FC wafunguka kuhusu Niyonzima
Michezo

Azam FC wafunguka kuhusu Niyonzima

Haruna Niyonzima, Kiungo wa Simba
Spread the love

KLABU ya Azam FC imethibitisha kuwa mpaka sasa hawajafanya mazungumzo yoyote na Haruna Niyonzima ambaye ni mchezaji wa timu ya Simba baada ya kuwapo kwa tetesi kuwa huwenda akatimka ndani kikosi hicho. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Niyonzima ambaye amekuwa katika wakati mgumu tangu alipojiunga na Simba katika msimu uliopita, hajaonekana mara nyingi uwanjani katika michezo ya Ligi Kuu Tanzania Bara baada ya kuwa katika majeruhi yaliyomuweka nje kwa muda mrefu na kuingia katika mgogoro na uongozi wa klabu hiyo.

Msemaji wa Azam FC, Jafari Idd amesema kuwa mpaka sasa hawajafanya mazungumzo na mchezaji huyo, lakini bado kwao dirisha lipo wazi na kama mwalimu atamuhitaji mchezaji wowote basi hawatosita kumchukua.

“Hao wachezaji bado hatujazungumza nao lakini huu ni mchezo wa mpira na lolote linaweza kutokea, sisi dirisha lipo wazi tuna msikiliza mwalimu anamuhitaji nani kama ni ndani ya nchi au nje ya nchi sisi tunamchukua tunampa mkataba.

“Naomba tuwaondoe presha wenye timu zao mwalimu akisema anamtaka yoyote kwenye klabu yoyote tutafanya naye mazungumzo na tutamchukua ili tupate huduma yake, lakini tunaomba hawa wachezaji wawe huru maisha yaona klabu zao ziondoe fikra hizo kwa sasa,” alisema Jafari Idd.

Azam FC ambao baada ya kufungiliwa kwa dirisha dogo la usajiri hapo jana, tayari walisha ingia kandarasi ya mwaka mmoja na mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Obrey Chirwa na huwenda wakafanya usajiri wa wachezaji wengi zaidi katika dirisha ili la usajili.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Meridianbet yaibukia Tandika, yafungua duka jipya

Spread the love BAADA ya kupita maeneo mbalimbali hatimae kampuni yaMeridianbet imeibukia...

BiasharaMichezo

Ukiwa na Meridianbet ni rahisi kuwa milionea

Spread the love  CARABAO Cup raundi ya 3 Uingereza inaendelea na mechi...

Michezo

Jezi ya Samatta iliyoifunga Liverpool kuuzwa Genk

Spread the love  KLABU ya KRC Genk ya nchini Ubelgiji imeamua kuanza...

BiasharaMichezo

Hii ndio historia ya El-Clasico, derby bora zaidi duniani

Spread the love  KILA nchi ina vilabu viwili hasimu na pinzani nje...

error: Content is protected !!