Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Michezo Azam Fc, Simba dimbani leo
Michezo

Azam Fc, Simba dimbani leo

Spread the love

 

Robo fainali ya tatu nan ne zitaendelea tena hii leo kwenye viwanja tofauti, ambapo Jijini Dar es Salaam mabingwa watetezi wa michuano hiyo klabu ya Simba itashuka Uwanjani kumenyana na Dodoma jiji FC kwenye Uwanja wa Mkapa jijini Dar es Salaam huku Azam Fc atakuwa ugenini mkoani Tabro dhidi ya Rhino Rangers. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea)

Mchezo utakaotangulia utakuwa wa Azam FC ambao utachezwa majira ya saa 10 jioni, na kufuatia na mchezo wa Simba dhidi ya Dodoma Jiji FC utakaopigwa majira ya saa 1 usiku.

Clatous Chama, kiungo wa klabu ya Simba

Washindi katika michezo hii miwili ya leo watakutana kwenye hatua ya nusu fainali ya michuano hiyo.

Prince Dube

Tayari Yanga imeshafuzu kwenye nusu fainali mara baada ya kuifunga Mwadui FC kwa mabao 2-0, na ambapo kwenye mchezo wa nusu fainali atavaana na Biashara United ambayo iliwaondosha Namungo FC.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Leo ni leo nani kutinga nusu fainali UEFA?

Spread the love HATIMAYE Jumanne ya UEFA imefika ambapo leo hii michezo...

Michezo

Anza Jumatatu yako na Meridianbet

Spread the love  IKIWA ni siku nyingine mpya kabisa ya Jumatatu baadhi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC, Yanga wazindua kadi  za kimataifa za uanachama

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) kwa kushirikiana na Klabu...

Michezo

TFF, Amrouche ngoma nzito

Spread the loveVIPENGELE vya mkataba wa kazi aliotia saini Kocha Mkuu wa...

error: Content is protected !!