Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Tangulizi Azam FC sasa kuvaana na pyramid ya Misri 
Tangulizi

Azam FC sasa kuvaana na pyramid ya Misri 

Spread the love

 

MARA baada ya kuibuka na ushindi wa bao 1-0, dhidi ya FC Horsed kutoka Somalia, klabu ya soka ya Azam FC, sasa itamenyana na Pyramid kutoka nchini Misri kwenye mchezo wa mzunguko wa kwanza wa kombe la Shirikisho barani Afrika. Anaripoti Hunda Mintanga TUDARCo … (endelea) 

Mchezo huo wa marejeano wa hatua ya awali ulipigwa leo, kwenye dimba la Azam Complex Chamazi, majira ya saa 10 jioni.

Ushindi huo utawafanya Azam FC, kuwa na jumla ya mabao 4-1, Kwenye michezo yote miwili ambayo walichezea kwenye Uwanja wa Azam Complex.

Pyramid ambao itakuwa mara yao ya tatu kushuka nchini kwenye michezo ya kimataifa dhidi ya timu kutoka Tanzania.

Mara ya kwanza timu hiyo kuja nchini ilikuwa kwenye mchezo wa kimataifa ambao ulichezwa kwenye dimba la Ccm Kirumba tarehe 27 octoba 2019, dhidi ya Yanga na kufanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 2-1.

Mara ya pili timu hiyo ilishuka nchini tarehe 17 Machi 2021, kwenye mchezo wa kombe la Shirikisho dhidi ya Namungo FC, nakuibuka na ushindi wa mabao 2-0.

Bao la Azam FC kwenye mchezo wa leo lilifunghwa na Ismael Kader dakika ya 38, kipindi cha kwanza na kuifanya timu hiyo kusonga mbele kwa hatua inayofuata.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

error: Content is protected !!