Saturday , 3 June 2023
Home Kitengo Michezo Azam Fc, Mwadui Dimbani leo
Michezo

Azam Fc, Mwadui Dimbani leo

Spread the love

LIGI kuu Tanzania Bara itaendelea tena leo kwa jumla ya michezo miwili kupigwa kwenye viwanja tofauti ambapo klabu ya Azam Fc itashuka dimbani kwenye mchezo wake wa sita wa Ligi Kuu dhidi ya Mwadui Fc kutoka Shinyanga. Anaripoti Kelvin Mwaipungu… (endelea)

Mchezo huo utapigwa majira ya saa 1 usiku kwenye Uwanja wa Azam Complex, Chamazi huku Azam Fc itamkosa beki wake Yakub Mohamed ambaye amechelewa kurudi kutoka kwenye majukumu ya timu yake ya Taifa ya Ghana.

Mchezo mwengine utaikutanisha timu ya Gwambina Fc ambao watatumia Uwanja wao wa nyumbani kwa mara ya kwanza baada ya kufungiwa na bodi ya Ligi kwa kuikaribisha Mtibwa Sugar kutoka Morogoro

Mpaka sasa Azam Fc wapo kileleni kwenye msimamo wa Ligi hiyo wakiwa na pointi 15 mara baada ya kucheza michezo mitano, huku wakifuatiwa na klabu ya Simba yenye pointi 13 sawa na Yanga ambao wanashika nafasi ya tatu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Dk. Mkwizu: Afrika tudumishe utamaduni

Spread the love  MWENYEKITI wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Mkoa wa...

Michezo

‘EONII’ kuteka tasnia ya filamu

Spread the love  UZINDUZI wa Filamu ya Kisayansi ya ‘EONII’ uliofanyika Mei...

Michezo

NBC Dodoma Marathon yazinduliwa, wakiambiaji 6,000 kushiriki

Spread the loveBENKI ya NBC imetangaza kufanyika kwa mbio kubwa za NBC...

Michezo

Rais Samia anunua tiketi 5000 Yanga vs USM Alger

Spread the loveRAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu...

error: Content is protected !!