Monday , 5 June 2023
Home Habari Mchanganyiko AZAKI zatakiwa kusimamia fedha za miradi vizuri
Habari Mchanganyiko

AZAKI zatakiwa kusimamia fedha za miradi vizuri

Spread the love

SERIKALI imezitaka Asasi za Kiraia (AZAKI) kusimamia vyema matumizi ya fedha za miradi, ili ziwanufaishe walengwa. Anaripoti Danson Kaijage…(endelea).

Wito huo umetolewa na Mwita Waitara, Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) wakati akizungumza na wakurugenzi wa AZAKI katika zoezi la kusaini mikataba ya ruzuku, lililofanyika jijini Dodoma.

Waitara amezitaka AZAKI hizo kuunda mifumo mizuri ya usimamizi wa fedha, ili  kudhibiti mianya ya ubadhirifu wa fedha za miradi.

Aidha, Waitara amezitaka AZAKI zote nchini kufanya kazi kwa kushirikiana na Maafisa wa Serikali za Mitaa pamoja na Halmashauri , kwenye maeneo yanayotekelezwa miradi .

 “Niwaombe sana,  hakikisheni mnafanya matumizi sahihi ya fedha za miradi na kuhakikisha walengwa halisi wanafikiwa na kufaidika na miradi  hiyo, pia mhakikishe mnawahusisha maafisa wa serikali za mitaa kwenye maeneo ya utekelezaji” amesema Waitara.

Pamoja na hayo, Waitara amesema serikali inatambua mchango mkubwa unaotolewa na Asasi za Kiraia nchini katika kusukuma mbele maendeleo vijijini, kuleta teknolojia mpya na rahisi kwa wananchi, sambamba na kupinga mila potofu na kandamizi miongoni mwa jamii hasa maeneo ya pembezoni.

Pia , Waitara ameziomba AZAKI kuwajengea uwezo wananchi pamoja na viongozi wa serikali za mitaa ili kuwawezesha kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi  kupitia mafunzo mbalimbali katika miradi, ili washirikiane kutatua changamoto zilizopo.

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Uwezeshaji wa AZAKI,  Francis Kiwanga, amesema mwaka huu watatoa ruzuku kiasi  cha Shilingi  11.7  Billioni kwa asasi za kiraia 154, ambazo zimekidhi vigezo  vya kupewa ruzuku ili wakatekeleze miradi yao.

Kiwanga amesema dhumuni la taasisi hiyo ni kuwekeza katika  utoaji wa ruzuku kwa AZAKI, na kuleta mabadiliko chanya yanayogusa maisha ya watanzania kupitia AZAKI zao.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Taasisi ya Tusonge kutoka Moshi, Aginata Rutazaa amesema watahakikisha wanaweka uwazi katika matumizi ya fedha ili ziweze kuleta tija kwa wahusika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Tunduma watenga 60 milioni kujenga machinjio ya kisasa

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma Imetenga kiasi cha Tshs Miloni 60...

Habari Mchanganyiko

Bilioni 17 kujenga bandari kavu Tunduma

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma iliyopo wilayani  Momba mkoani Songwe imepatiwa...

Habari Mchanganyiko

Bandari ya Kigoma kuongezewa uwezo wa kutoa huduma zake

Spread the love  SERIKALI kupitia mamlaka ya Bandari nchini (TPA), imewekeza takribani...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kifo cha mwanafunzi UDOM: Tume yamsafisha naibu waziri

Spread the loveTUME ya Haki za Binadamu na Utawala Bora nchini (THBUB),...

error: Content is protected !!