Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari Aucho, Fei Toto kuikosa Azam FC, Bangala Farid hati hati
HabariMichezo

Aucho, Fei Toto kuikosa Azam FC, Bangala Farid hati hati

Spread the love

 

VIUNGO wa klabu ya Yanga Feisal Salum ‘Fei Toto’ sambamba na Khalid Aucho hawatakuwa sehemu ya kikosi cha klabu hiyo kitakachoshuka dimbani kwenye mchezo dhidi ya Azam FC. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea)

Mchezo huo wa Ligi Tanzania Bara mzunguko wa pili utapigwa kesho tarehe 6 Aprili 2022, majira ya saa 2:15 kwenye dimba la Azam Complex Chamazi.

Feisal anaukosa mchezo mara baada ya wiki iliyopita kupama maumivu alipokuwa kwenye kambi ya timu ya Taifa na kupewa mapumziko ya siku 14.

Akitoa taarifa juu ya wachezaji hao, kocha msaidi wa klabu ya Yanga Cedric Kaze aliwaambia wanahabari kuwa viungo hao wawili hawatokuwa sehemu ya mchezo wa kesho.

“Kuna wachezaji ambao tutawakosa kwenye mchezo wa kesho Aucho, Feisal wao bado wanauguza majeraha yao, kutokana na kuumia .” Alisema kocha huyo.

Kwa upande wa Yanick Bangala na Farid Mussa, kocha huyo msaidi alisema kuwa kwenye mazoezi ya leo ndio watajua kama wanaweza kuwatumia wachezaji hao kutokana na kutokuwa sawa siku za hivi karibuni.

“Kuna wachezaji kama Bangala na Farid wao bado hatujajua kama tutawatumia, kutokana na Farid kuumwa ghafla wiki hii na kukimbizwa hospital na Bangala nae aliumia siku mbili zilizopita mazoezi”- Aliongezea Kaze

Yanga wanaingia kwenye mchezo huo huku wakiwa na rekodi ya kucheza mechi 18 kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara na mpaka sasa kuwa timu pekee ambayo haijapoteza mchezo katika klabu 16 zainazocheza Ligi.

Kwenye mchezo wa mzunguko wa kwanza Azam Fc ikiwa chini ya George Lwandamina walikubali kichapo cha mabao 2-0, dhidi ya Yanga, mchezo uliopigwa kwenye dimba la Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam.

Mchezo huo wa kesho kwenye dimba la Azam Complex, utakuwa mchezo unaowakutanisha Azam FC na Yanga mara tatu kwenye uwanja huo, huku katika mara mbili Yanga akifanikiwa kuondoka na matokeo ya ushindi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!