Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Michezo Aucho, Djuma Shabani hatihati kuikosa Ligi ya Mabingwa
MichezoTangulizi

Aucho, Djuma Shabani hatihati kuikosa Ligi ya Mabingwa

Khalid Aucho, kiungo wa klabu ya Yanga
Spread the love

 

KUELEKEA mchezo wa awali wa michuano ya Ligi ya Mabingwa Barani Afrika Afrika, uongozi wa klabu ya Yanga umefunguka kuwa huwenda ukawakosa wachezaji wake watatu kutokana na kukosa hati ya kimataifa ua uhamisho. Anaripoti Mintanga Hunda, TUDARCo…(endelea)

Mchezo huo wa hatua ya awali utapigwa kwenye dimba la Benjamin Mkapa, jijini Dar es Salaam, Septemba 12, mwaka huu ambapo Yanga itashuka dimbani dhidi ya Rivers United ya Nigeria.

Akithibitishja taarifa hiyo Msemaji wa klabu ya Yanga, Haji Manara amesema kuwa mpaka sasa hati za wachezaji Khalid Aucho, Djuma Shabani na Fiston Mayele bado hazijatumwa kutokana na kuwepo kwa mivutano kwenye timu zilizotoka.

“Tutawakosa wachezaji wetu watatu, ambao ni Aucho, Mayele pamoja na Djuma Shabani”

“Kukosekana kwa wachezaji hawa haikuwa makossa ya klabu ya Yanga, Majele na Djuma Shabani mikataba yao ilikuwa inaisha tarehe 31, na tulipopeleka maombi ya hati zao waliatuambai tusubili hadi tarehe hiyo.” Alisema Manara

Djuma Shabani, mlinzi wa kulia wa Yanga

Aidha Manara alizungumzia kilichokwamisha hati ya usajili ya Aucho na kufungukuwa kuwa mchezaji huyo alikuwa kwenye migogoro na klabu yake aliyotoka nchini Misri hivyo walizuia kibali chake.

“Aucho alikuwa na mgogoro mkubwa na klabu yake, hakupewa mshahara wake kwa muda mrefu kidogo na baadae wakaenda Fifa wakaambiwa huyu ni mchezaji huru na wao wakashindwa kutupa hiyo hati kwa muda uliopangwa.”

Manara aliendelea kufafanua kuwa klabu hiyo, ilifanya juhudi ya kuwasiliana na Caf kuhusu hati za wachezaji hao, lakini hawajapata majibu yanayoweza kuwaruhusu wachezaji hao kucheza

Fiston Mayele, mshambuliaji wa Yanga

“Tulifanya taratibu za kuwasiliana na watu wa Caf hawajatoa majibu ya kuwaruhusu wachezaji wetu kucheza, na tumeshawaandikia Fifa na tunaamini watatoa hati za wachezaji hao, kupitia Tff.” Alifunguka Manara

Wachezaji hao wote watatu wamesajiliwa kwenye dirisha kubwa la usajili lililofungwa Agosti 31, na wataitumikia klabu ya Yanga, kwenye msimu ujao wa mashindano 2021/22

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

error: Content is protected !!