Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Askofu Mchamungu: Mrema alikuwa kiongozi wa kipekee
Habari za SiasaTangulizi

Askofu Mchamungu: Mrema alikuwa kiongozi wa kipekee

Spread the love

ASKOFU Msaidizi wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Henry Mchamungu amesema kuwa Hayati Agustino Mrema alikuwa kiongozi wa kipekee kutokana uweledi aliouonesha katika nyadhifa mbalimbali alizozishika enzi za uhai wake ndani na nje ya Serikali. Anaripoti Juliana Assenga TUDARCo …  (endelea)

Mchamungu ametanabaisha hayo leo tarehe 24 Agosti, 2022  kwenye ibada ya mazishi ya mwanasiasa huyo mkongwe iliyofanyika katika Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Agustine iliyopo Salasala jijini Dar es Salaam.

Katika mahubiri yake Askofu huyo amesema kuwa upekee wa mwanasiasa huyo, ulianzia alipokuwa Mbunge wa Moshi katika jimbo la Vunjo, kwa kuhakikisha watu katika eneo lake wanaishi katika mazingira mazuri kwa kutengeneza miundombinu imara.

“Mrema mwaka 1985 akiwa kama mbunge alijitahidi kuhakikisha watu walioishi katika eneo lake wanapata miundombinu bora hali iliyoimarisha maendeleo eneo hilo,” alisema Askofu huyo.

Ibada hiyo ya misa takatifu ilihudhuriwa pia na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa pamoja na Waziri Mkuu mstaafu Fedrick Sumaye na wanasiasa mbalimbali.

Aidha, Askofu huyo aliendelea kusema kuwa enzi za uhai wake akiwa kama Waziri alipata sifa kubwa kwa kuanzisha vikundi mbalimbali vya ulinzi ili wananchi waishi kwa amani.

“Mrema kama waziri alikuwa shujaa katka usalama wa mambo ya ndani. Na ndipo kipindi cha utawala wake vikundi vya ulinzi shirikishi (sungusungu) vilipoanzishwa ili kuhakikisha watu wanaishi kwa amani na usalama,” alisema Askofu Mchamungu.

Mrema alifariki dunia tarehe 21 Agosti, 2022 katika hospitali ya Taifa Muhimbili ambako alikuwa amelazwa tangu tarehe 16 Agosti, 2022 akipatiwa matibabu kutokana na matatizo ya mapafu.

Mwili wa mwanasiasa huyo mkongwe nchini unasafirishwa leo jioni kwenda Marangu mkoani Kilimanjaro ambapo utapumzishwa katika kijiji cha Kiraracha kesho tarehe 25 Agosti 2022.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Bajeti ya Ikulu 2024/25 kuongezeka, bunge laombwa kurudhia Sh. 1.1 trilioni

Spread the love  WIZARA ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

error: Content is protected !!