Tuesday , 19 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Askofu Kilaini alaani Klabu ya Simba kutumia msalaba kwa dhihaka
Habari MchanganyikoTangulizi

Askofu Kilaini alaani Klabu ya Simba kutumia msalaba kwa dhihaka

Spread the love

ASKOFU Msaidizi wa Jimbo Katoliki la Bukoba, Methodius Kilaini amelaani kitendo cha klabu ya Simba kutumia msalaba kufanya dhihaka na kusema ni “dharau na kufuru kubwa kwa waamini wakristu na wote wanaoamini walikombolewa katika msalaba huo.”

Itakumbukwa kuwa katika tamasha la Simba Day lililofanyika jana Jumatatu tarehe 8 Agosti, 2022, msaani Tunda Man aliingia katika uwanja wa Benjamini Mkapa akiwa amebebwa katika jeneza pamoja na msalaba uliokuwa na maneno ya dhihaka kwa watani wao wa jadi Yanga yaliyosomeka “Kifo cha Utopolo.”

Askofu Kilaini amesema katika andiko lake kwenye akaunti yake ya Facebook kuwa “tendo hili ni kufuru kwa ishara zilizotakatifu kwa Imani yaani Msalaba. Kutumia msalaba kudhihaki ni dharau na kufuru kubwa kwa waamini wakristu na wote wanaoamini kwamba walikombolewa katika msalaba huo.

Ameendelea kusema “ni tusi kubwa kwao.”

Mbali na matumizi ya msalaba pia amelaani uvaaji wa mavazi yanayofanana na yale yanayovaliwa katika ibada takatifu na kusema “ni kuzifanya ibada za Kikristo kichekesho. Inasikitisha sana. Sikutegemea tumefikia hatua hiyo.”

Askofu Kilaini amesema ni matumaini yao kuwa uongozi wa Klabu ya Simba utalaani kitendo hico na kuomba msamaha kwa waamini wakristo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Diwani, wananchi wengine 463 wahama Ngorongoro

Spread the loveMakamu mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Ngorongoro ambaye pia...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Shule zafungwa kutokana na ongezeko la joto

Spread the loveSUDAN Kusini imeamuru kufungwa kwa shule zote kuanzia leo Jumatatu,...

Habari Mchanganyiko

Bunge laja na Marathon kuchangia ujenzi wa sekondari

Spread the loveBUNGE la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linatarajia kukusanya fedha...

error: Content is protected !!