WABUNGE wa Chama tawala nchini Tanzania- Chama Cha Mapinduzi (CCM), Askofu Josephat Gwajima wa Kawe, Jerry Silaa wa Ukonga na Humphrey Polepole wameitikia wito wa kufika kuhojiwa na kamati ya maadili ya chama hicho. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).
Askofu Gwajima na Silaa, wanahojiwa leo Ijumaa tarehe 3 Septemba 2021, makao makuu ya CCM jijini Dodoma na kamati hicho inayoongozwa na mwenyekiti wake, Hassan Mtenga.
Mbali na wabunge hao ambao wanatumikia adhabu ya kutohudhuria mikutano miwili ya Bunge, mwingine ni Humphrey Polepole ambaye ni Mbunge wa Kuteuliwa.

Askofu Gwajima na Silaa tayari wamekwisha kufika na wanasubiri kuanza kuhojiwa huku Polepole aliyewahi kuwa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho yeye amekwisha kuhojiwa na kuondoka.
Endelea kufuatilia MwanaHALISI TV, MwanaHALISI Online na mitandao yetu ya kijamii kwa habari na taarifa mbalimbali
HAO WANAMCHEZA SHERE RAIS SAMIA HASSAN SULUHU HAWAUKUBALI UONGOZI WAKE HATA WAKATI WA UTAWALA MWA MAGU HAWAKUWA NA HESHIMA NA MAKAMO WA RAIS. DAWA YAO HAO NI “KUWAKOLIMBA” MAPEMA ILI IWE FENDISHO KWA WENGINE WAKIACHWA WATAZALISHWA WENGI ZAID KTK HILO GROUP LA WATU WATATU NA KUWA (666) KWAHIIYO CCM KAMA MNAHISTORIA YA KUWAKOLIMBA WASALITI MSIWAACHE HAO NI MAADUWI WA UONGOZI WA AWAMU YA (6) …
Acha kuwatisha watanzania wenzako hayo maneno unayoandika unaushaidi. Acha kamati inafanye kazi yake