Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Askofu Gwajima, Jerry Silaa waondolewa kwenye kamati
Habari za SiasaTangulizi

Askofu Gwajima, Jerry Silaa waondolewa kwenye kamati

Spread the love

 

ASKOFU Josephat Gwajima ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Kawe na Jerry Silaa wa Jimbo la Ukonga mkoani Dar es Salaam kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) na ambao ni wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge wameondolewa kwenye kamati hiyo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Uamuzi huo umetolewa leo Agosti 24, 2021 hadi itakapoamuliwa vinginevyo Bungeni jijini Dodoma.

Askofu Josephat Gwajima na Jerry Silaa wameitwa mbele ya kamati hiyo wakituhumiwa kusema uongo, kushusha hadhi na heshima ya Bunge.

Kamati hiyo ina jumla ya wajumbe 24 wakiwamo Gwajima na Silaa na sasa imebaki na wajumbe 22 baada ya hatua hiyo.

Askofu Gwajima alianza kuhojiwa jana tarehe 23 Agosti, 2021 na kamati hiyo kwa zaidi ya saa mbili na tarehe 25 Agosti, 2021 ataendelea kuhojiwa wakati Silaa anahojiwa leo mbele ya kamati hiyo inayoongozwa na Mwenyekiti Emmanuel Mwakasaka.

Mwakasaka amesema unapotuhumiwa mara nyingi, wewe ndio mshtakiwa.

“Hivyo zipo taratibu zinafuata. Kama wewe ni mtuhumiwa huwezi kuwa hakimu kwenye kesi yako mwenyewe,”amesema Mwakasaka huku akiongeza kuwa, tayari wajumbe hao wameondolewa katika kamati.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

error: Content is protected !!