Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Askofu Gwajima amfananisha Rais Magufuli na Nabii
Habari za Siasa

Askofu Gwajima amfananisha Rais Magufuli na Nabii

Spread the love

ASKOFU Mkuu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Dk. Josephat Gwajima amemfananisha Rais John Magufuli na Nabii. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Akichangia hoja katika mkutano wa wadau wa sekta ya madini uliofanyika leo tarehe 22 Januari 2019 jijini Dar es Salaam, Askofu Gwajima amesema Rais Magufuli amekuwa kama nabii.

“Ahsante sana rais leo umekuwa kama nabii, wakati nimekaa hapa nilisema itawezekanaje nitoke hapa bila kuongea, ingekuwa shida,” amesema Gwajima.

Akichangia kuhusu changamoto zianzoikabili sekta ya madini hapa nchini, Askofu Gwajima ameishauri serikali kuunda timu ya watu wenye uwezo na ushawishi wa kumudu siasa za kibiashara katika kiwango cha kimataifa hasa kwenye kutafuta masoko ya madini nje ya nchi.

“Si kweli hakuna soko la madini, sababu dhahabu yenyewe ni fedha ukiwa nayo ni fedha, isipokuwa tu nilikuwa nashauri, uwe na watu wenye exposure na siasa ya madini, kuunda watu wenye akili na wenye exposure ambao wanaweza kuziikia nchi mbalimbali dunia kutafuta masoko

Kuhusu changamoto ya uwepo wa kodi katika biashara ya madini, Gwajima amesema hashauri kupunguzwa kwa kodi bali serikali iwapunguzie kiwango cha kodi kwa wachimbaji wenye kiwango kidogo cha madini.

“Nilipita Mwadui njiani Maganzo nilishangaa kweli, nikapaki gari watu wakasema huyu Gwajima wakanifuata wakitaka kuniuzia dhahabu, ndani ya saa moja nililetewa bakula la ilog tano limejaa Almasi. Hizi kama zingelipiwa ushuru nchi yetu ingefika mbali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!