Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Askofu Desmond Tutu afariki dunia, Rais Ramaphosa amlilia
Kimataifa

Askofu Desmond Tutu afariki dunia, Rais Ramaphosa amlilia

Spread the love

 

ASKOFU mkuu mstaafu nchini Afrika Kusini, Desmond Tutu amefariki dunia leo Jumapili, tarehe 26 Desemba 2021. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Tutu amefikwa na mauti akiwa na miaka 90 akikumbukwa kwa mapambano makubwa aliyoyafanya nchini humo ya ubaguzi wa rangi.

Alikuwa akisumbuliwa na saratani ya tezi dume aliyoipata mwishoni mwa mwaka 1990.

Katika kipindi cha miaka ya hivi karibuni, Askofu Tutu aliyeipigania Afrika Kusini akiwa na Hayati Nelson Mandela, Rais wa Taifa hilo wa kwanza mweusi, alikuwa akilazwa mara kwa mara hospitalini.

Tutu alishinda tuzo ya amani ya Nobel mwaka 1984 ambapo Rais wa taifa hilo, Cyril Ramaphosa amesema, huo ni msiba mwingine mkubwa kwa Waafrika Kusini mashuhuri wakiondoka kwenye sura ya dunia.

Amesema, Askofu Tutu alikuwa mtu mashuhuri ndani na nje ya Afrika Ksuini, “kwetu sisi ametuachia urithi mkubwa uliokombolewa, utakaodumu vizazi hadi vizazi.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!